
Dk Gwajima ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 17, 2021 katika Kijiji cha Kyatunge wilayani Butiama mkoani Mara, na kueleza kuwa Askofu Gwajima amekuwa akitoa taarifa za kupotosha kwa makusudi, jambo linaloivuruga wizara na Serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo.
"Gwajima ni ndugu yangu, ni shemeji yangu kabisa, lakini mimi ni waziri nimekula kiapo cha kutumikia nchi yangu sio kumtumikia shemeji yangu. Mimi ndiye msemaji wa masuala ya afya nchini, nimechoka kuvuruguwa. Naagiza akamatwe popote alipo ahojiwe juu ya haya madai yake na hatua zichukuliwe" amesema
SOMA ZAIDI HAPA; CHANZO MWANANCHI
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464