Header Ads Widget

TIA YAWAPONGEZA SHULE YA ANDERLEK NA ROCKEN HILL KATIKA MALEZI NA MAADILI KWA WANAFUNZI

 Mkurugenzi wa taasisi za shule  ya sekondari  Anderlek Ridges,  shule ya msingi Rocken Hill na Rocken Hill Academy. Alexander Kazimili akitoa  ushauri kwa wazazi juu ya malezi.

Na Kareny Masasy,Kahama

WATOTO wametakiwa  kuongoza na wazazi  wao   katika ulimwengu huu wa kidigital  na sio wazazi  kuwapa malezi ya kuwadekeza  hali ambayo imewakuta watoto wengi  nakuwafanya kuharibikiwa  katika mstakabali wa maisha yao yote.

Hayo yamesemwa na  Naibu  makamu mkuu wa chuo cha Mipango,fedha na utawala (TIA) dk  Hassanal Issaya  alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 15 ya shule ya sekondari  Anderlek Ridges na  shule ya msingi Rocken Hill na Rocken Hill Academy.

Dk Issaya amesema wazazi wengi wameonekana kuwapenda watoto wao zaidi hadi kuharibikiwa wanatakiwa waelezwe maisha na namna ya kuishi  kumbuka watoto wamekuwa na ufahamu   mkubwa  ukiwapa kuigiza  kwa vitendo maisha yalivyo wanaweza kinachotakiwa ni kuwapatia muongozo mzuri wa wenye maisha bora.

 “Dunia ya sasa ipo kwenye utandawazi  na hautakiwi kutumia mabavu   la sivyo dunia itakuacha  na wanafunzi wanamaliza  watakwenda majumbani  na mitaani watakutana na utandawazi   kitu cha ushauri wazazi wawe makini  katika malezi  na simu zitumike kuongeza ujuzi wa elimu sio mambo mengine”alisema dk Issaya.

Dk Issaya amesema   katika maisha hakuna kubahatisha  na mtu lazima uwe na ndoto  kwa kuweka malengo  yenye mikakati dhabiti na kuchukua hatua ili kuyafikia malengo hayo yatimie.

“Hivi sasa watoto wengi wanakimbilia mziki zamani tuliona ni uhuni  na ukicheza mpira nakurudi jioni mzazi anakuchapa nakulazimishwa upende anachotaka mzazi  hivyo muwaache wanachokipenda na kukiendeleza huko nako wanaweza kuwa matajiri.”amesema dk Issaya.

Mkurugenzi wa taasisi za shule hizo Alexander Kazimili  akieleza katika  mahafali hayo aliwataka  wanafunzi yale waliyojifunza shuleni wakayaendeleze huko mitaani waendako kwani wazazi wamewapa zawadi kubwa  na bora  ya Elimu ambayo ni  rasilimali  isiyoisha.

“Maisha ni magumu kama una Elimu na Ujuzi  ni rasilimali tosha  na bahati  wanayoitaka ni kuvaa  viatu vya kujishughulisha kwa bidii  kwani vijana wengi wanataka maisha ya kubahatisha  na  wakati wote muda uko sahihi na utandawazi uliopo mtaji wake ni akili “alisema Kazimili.

Mkurugenzi wa shule ya sekondari Anderlek Ridges   Godwin Ng’osha amesema  wahitimu wa kidato cha nne ni  161  na mkurugenzi wa shule ya msingi  Rocken Hill Zephania Madaha amesema  wahitimu ni 174 na walieleza  wanafunzi wamekuwa wakifundishwa maadili  ya kidini na nidhamu katika maisha watakayo yapitia.

Naibu  makamu mkuu wa chuo cha Mipango,fedha na utawala (TIA) dk  Hassanal Issay mgeni rasmi .
Naibu  makamu mkuu wa chuo cha Mipango,fedha na utawala (TIA) dk  Hassanal Issaya 

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Anderlek wakiwa katika Mahafali.


 

Post a Comment

0 Comments