Header Ads Widget

UWT TAIFA WAANZA ZIARA MKOA WA SHINYANGA, WASISITIZA SUALA LA MAADILI


    Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Zainab Shomari akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Jitegemee Kata ya Maganzo Wilaya ya Kishapu Mkoa wa Shinyanga baada ya kutembelea shule hiyo alipokuwa kwenye ziara ya kukagua ujenzi wa shule mpya ya Msingi Nguzo.

Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Zainab Shomari akiwa na viongozi wengine wa Chama
Na shinyanga Press Club Blog

Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Zainab Shomari amewataka wanawake  kuwalea watoto wao kwa kufuata misingi ya maadili ikiwa ni pamoja na kuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia na  kuacha kufumbia macho matukio ya ukatili wa kijinsia yanapotokea. 

Hayo ameyasema leo Agosti 25/2023  wakati akizungumza na wakazi wa Kata ya Idukilo na Maganzo kwa nyakati tofauti Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga ,ambapo amesema maadili yameporomoka katika jamii na kuchangia vitendo vya ukatili kuongezeka ukiwemo ubakaji na kulawiti watoto.

Amesema wanawake ni jeshi kubwa wanapaswa kuwa imara katika kukemea vitendo hivyo ili kuvikomesha kwa kushirikiana na  jamii na wadau wengine wa kupinga vitendo hivyo kwa kuunganisha nguvu ya pamoja katika kupaza sauti.

Katika hatua nyingine Makamu Mwenyekiti UWT Taifa amewataka wakinamama kuachana na mikopo ambayo inasababisha kuchukuliwa mali zao na wengine kukimbia familia kutokana na mikopo umiza.

Naye Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Shinyanga Santiel Kirumba amesema kutokana na wakinamama wengi kuumizwa na mikopo umiza serikali imeamuwa kuja na mpango mwingine ambao utawezesha hata mtu  binafsi kupata mkopo  hatua ambayo itakuwa ni mkombozi kwa wanawake. 

Amesema kuendelea kuficha matukio kuna changia matukio hayo kuendelea kutokea na kuathiri watu wengi ikiwa ni pamoja na kuwanyima haki watoto kuendelea na elimu . 

Katika ziara ya viongozi wa UWT Taifa ambao ni Mwenyekiti Mary Chatanda na Makamu wake Zainab Shomari imegawanyika katika makundi nane kwa lengo la kuwafikia wananchi Vijijini kwa haraka katika Kata zote za Wilaya ya Kishapu,ambapo atakuwa na ziara ya siku nne Mkoani Shinyanga na atatembelea Wilaya zote .

                Wanafunzi wa shule ya msingi Jitegemee wakimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa

   Mwenyekiti wa UWT Taifa Mary Chatanda akivishwa vazi la kimila na mmoja wa viongozi wa kimila Kishapu mara baada ya kuwasili Wilayani humo kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi kukagua shughuli za maendeleo.

           Kiongozi wa kimila Kishapu Fransisca Bahame akimkaribisha Mwenyekiti wa UWT Taifa Wilaya ya Kishapu 

      Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Zainab Shomari akizungumza na wakazi wa Maganzo pamoja na Kata jirani Idukilo,Mwaduilohumbo na Songwa kwenye mkutano wa hadhara

Wakazi wa Kata ya Maganzo wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Zainab Shomari
    Madarasa ya shule mpya ya nguzo Kata ya Maganzo


Mjumbe wa NEC Taifa  kupitia Mkoa wa Shinyanga Gasper Kileo akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Jitegemee ambapo amewataka kuzingatia masomo ili wafikie ndoto zao

Wakazi wa Kata ya Maganzo wakiwa kwenye mkutano wa hadhara
 

Post a Comment

0 Comments