Header Ads Widget

KUTEMBEA UMBALI MREFU KWA WAJAWAZITO NA WATOTO KUTAFUTA HUDUMA ZA AFYA YATATULIWA




 

Zahanati ya Saeni yazinduliwa kuokoa vifo vya  mama na mtoto 

Julieth Ngarabali ,Kibaha

WAJAWAZITO na watoto wa umri wa miaka 0 mpaka nane katika kata ya Misugusugu mjini Kibaha wameondokana na adha ya kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita  20 kufuta huduma za afya huko Mlandizi Kibaha Vijijini kufuatia kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa zahanati ya kisasa ya Saeni na kuanza kutoa huduma zote ikiwemo ya afya ya uzazi.


Wajawazito hao ni miongoni mwa Wananchi takribani 14,000 wanaoishi kwenye mitaa mitatu ya Saeni, Zogowale na Jonung'ha katika kata ya Misugusugu mjini Kibaha ambao awali walikabiliwa na changamoto ya kutembelea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Akizindua kuanza huduma za afya katika zahanati ya Saeni Mbunge jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka amesema kuanza kwa huduma hizo ni jitihada za Wananchi wa maeneo hayo kujitolea nguvu zao wenyewe ikiwemo halmashauri na  Serikali.

Koka amesema wananchi walipochoshwa na adha ya kutembea umbali mrefu walitafuta eneo la ujenzi wa mradi huo ambapo katika kuwaunga mkono alichangia sh  Milioni 6.5 kwa ajili ya kununua mifuko ya saruji ya kuanzia ujenzi huo na wadau wengine wakaunga jitihada hizo.

" Mnakumbuka wakati nilipoomba ridhaa ya kuwa Mbunge wenu mliniambia mna shida ya maji, barabara na zahanati niliwapigia magoti kuwaomba kuwa tutazitatua na kweli tumeshirikiana  halmashauri pamoja na  Serikali ya CCM leo tumekamilisha vyote.

 Mbunge Koka  amesema   zahanati ndio hii imefunguliwa  nani mkombozi mkubwa  hapa kwenye vijiji vyetu  itasaidia wajawazito kuwahi matibabu na hata watoto kuhudhuria kliniki .

Mbunge Koka alibainisha lengo lake kubwa ni kuwatumikia wananchi hivyo atahakikisha anaendelea kushirikiana nao jimboni humo kwenye sekta zote ili waweze kuondokana na kero ambazo wamekuwa wakizipata.

Awali mganga mfawidhi wa halmashauri ya mji Kibaha Peter Nsanya amesema mradi wa Ujenzi zahanati hiyo mpaka kukamilika umegharimu sh Millioni  181  zilizotokana na nguvu za wananchi  ikiwemo mfuko wa mbunge ikiwemo halmashauri na Serikali kuu.
 

"Mradi wa ujenzi huo utaweza kusaidia zaidi hasa kwa upande wa huduma za mama na mtoto ambao walikuwa wanapata shida ya kusafiri umbali mrefu  kuzifuata huko Mlandizi  huduma za afya  hata hivyo bado upo upungufu wa viti " amesema  dk  Nsanya.

Aidha Diwani wa kata ya Misugusugu Upendo Ngonyani amemshukuru Mbunge Koka kwa namna anavyoshirikiana na Wananchi kuzitatua changamoto zilizopo na pia kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo.
 

Baadhi ya wakazi wa mitaa hiyo wameshukuru mradii huo kuanza kazi kwani itaongeza chachu ya wajawazito wengi kuanza kliniki mapema na kupata elimu ya lishe ikiwemo  kinga ya maradhi mbalimbali pamoja na  saratan ya mlango wa uzazi na  wengine kupata tiba kwa wakati.

Post a Comment

0 Comments