TCRS YASIMAMIA KIKAO CHA KUPOKEA NA KUJADILI TAARIFA YA KAMATI ZA PETS
KISHAPU
Na Frank Mshana,
Changamoto ya baadhi ya Jumuiya
za watumia maji yaani
CBWSO Wilayani Kishapu kutowasomea wananchi mapato na matumizi imetajwa kuwa
imeanza kupungua baada ya Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na kutoa
huduma za kijamii kwa watu wenye mahitaji ikiwemo kuwezesha jamii
kuboresha miundombinu ya usafi na maji katika maeneo yenye changamoto ya
ukame na uhaba wa maji.

TCRS
imeziwezesha kamati za kufuatilia matumizi ya rasilimali za umma katika,
uendeshaji wa miradi ya maji wilayani Kishapu Mradi ambao
unafadhiliwa na shirika la Foundation for Civil Society (FCS) na
kutekelezwa na shirika la TCRS kwenye vijiji 10 vilivyoko kata 5 za Bubiki,
Bupigi, Ukenyenge, Lagana na Mwakipoya.
Mwanamina Mavura ambaye anaratibu
mradi wa ‘’UWAZI NA UWAJIBIKAJI’’ unaotekelezwa na shirika la TCRS kwa ufadhili
wa Shirika la Foundation For Civil Society (FCS) wilayani Kishapu amesema
malengo ya mradi huo ni kuona jamii inawajibika ipasavyo katika kusimamia na
kufuatilia bajeti ya sekta ya maji na kuwakumbusha viongozi juu ya uwazi na uwajibikaji
katika kusimamia na kulinda miundombinu ya maji ili kuhakikisha kunakuwa na
uendelevu na upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ili kupunguza athari
zinazotokana na ukosefu wa maji safi na salama.Baadhi ya viongozi waliohudhuria
kikao hicho kilichofanyika tarehe 20/10/2023 wakiwemo madiwani na watendaji wa halmashauri ya wilaya
wamezungumzia changamoto ya kukatika maji mara kwa mara hasa kwenye miradi ya maji ya ziwa Victoria
na kuziomba mamlaka za maji KASHWASA na RUWASA kufuatilia changamoto hiyo na
kupata ufumbuzi wa kudumu ili kutatua kero hiyo ambayo imetajwa kuleta madhara
kwenye jamii.Nao baadhi ya wajumbe wa kamati
za PETS wamewashauri viongozi wa jumuia za watumia maji (CBWSO)
kushirikiana na PETS kama timu moja ili
kusaidia upatikanaji wa taarifa muhimu wakati wa ufuatiliaji na kuwataka
viongozi wa vijiji kuitisha mikutano ya hadhara kusikiliza kero za wananchi na
kuwasomea mapato na matumizi ya miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo
yao.Nao baadhi ya viongozi wa kata na
vijiji wamezishauri mamlaka za maji kuanza mchakato wa kuleta teknolojia ya
kisasa ya malipo ya kabla kwenye Ankara za maji au mfumo wa matumizi ya token
ili kutatua changamoto ya 1` ulimbikizaji wa bili za maji haswa kwenye baadhi
ya taasisi za Serikali.Kuhusu malalamiko ya bei za
Ankara za maji, kaimu Meneja wa RUWASA wilaya ya Kishapu Mhandisi Christopher
Daniel Damas amewashauri wananchi waliopitiwa na mtandao wa maji kujitahidi
kuvuta maji majumbani mwao ili idadi ya watumia maji iongezeke huku Afisa
Maendeleo wa Wilaya ya Kishapu Bwana Joseph Swalala akionekana kusikitishwa na
mwamko mdogo wa wananchi kuunganisha maji majumbani mwao.
Aidha mwezeshaji wa kikao hicho,
Bwana Evance Mvamila amewashauri wataalamu wa RUWASA wanapoandaa (design)
miradi ya maji kuhakikisha wazingatia malengo ya muda mrefu mbele ya ongezeko
la watu kwa lengo la haklikisha miradi ya maji inayojengwa inakidhi idadi ya
watumiaji kwa kipindi kirefu.
Baadhi ya Madiwani wa halmashauri
ya wilaya ya Kishapu kutoka kata za
mradi, hawakubaki nyuma wakati wa mkutano huo na wamesisitiza kuwa uwazi na
uwajibikaji ni nguzo muhimu ya
uendeshaji na usimamizi wa miradi ya maji ili kuhakikisha upatikanaji wa maji
safi na salama na uendelevu wa miradi.Mwenyekiti wa kamati ya Elimu, Afya na Maji wa
halmashauri ya (W) ya Kishapu Bwana Joel Ndetoson ambaye pia alikuwa ni
mwenyekiti wa kikao hicho amelipongeza shirika la TCRS kwa kazi kubwa ya
kuhakikisha changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa Wilaya ya
Kishapu zinapungua huku akitoa ushauri kwa CBWSO kudhibiti mapato yatokanayo na
mauzo ya maji pamoja na utatuzi wa changamoto zingine zilizojitokeza
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464