Header Ads Widget

KIJIJI CHA KILIMAWE SHINYANGA CHAANZA KUPATA MAJI SAFI NA SALAMA, ILANI YA CCM YATEKELEZWA



Viongozi na wananchi  wa kijiji cha Kilimawe wakifurahi huduma ya maji

Na Kareny Masasy, Shinyanga

WAKAZI wa kijiji cha kilimawe kata ya Mwantini  halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wameanza kunufaika na mradi wa maji safi  chanzo chake ni kutoka  ziwa Victoria mbapo wameondokana na changamoto ya kununua maji ndoo sh 500  hadi 1000.

Hayo yamesemwa jana na wakazi hao mbele ya Mbunge viti Maalum  mkoa wa Shinyanga Santiel Kirumba ambaye alikuwa ameambatana na viongozi wa umoja wa wanawake Tanzania (UWT) wa chama cha Mapinduzi  mkoa wa Shinyanga  kwaajili ya kujionea utekelezaji wa miradi ya maji vijijini.

Mbunge Kirumba amesema kazi imefanywa vizuri na wakala wa maji safi na mazingira vijijini (Ruwasa) ambayo mradi umekamilika kwa kutekelezwa siku 170  na fedha zimebaki  na leo tarehe 30,Nomvemba,wananchi wananufaika rasmi.  .

Mbunge Kirumba  amesema kitu ambacho kimemfurahisha zaidi ni  fedha kubaki katika mradi huo na amewaeleza wananchi  maji hayo ni hazina wayatumie vizuri kwa kutunza miundombinu kwani Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa maono yake kipaumbele ni Elimu,afya na maji.

“Serikali imeleta fedha nyingi  kwenye miradi ya maji tunachotaka maeneo yote kwenye taasisi  kama shule na Zahanati yapate maji safi na salama waondokane na changamoto ya kutafuta  maji ambayo siyo safi kazi imefanywa ya kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi”amesema Mbunge  Kirumba.

Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Shinyanga  Grace Samweli amesema  wanasimamia ilani ya (CCM) kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama hivyo wanaume nao wanatakiwa kupongeza juhudi hizi ambazo zilikuwa zikiwafanya wanawake kutafuta maji nyakati za usiku nakucha kufanya shughuli za kijamii.

Katibu wa UWT mkoa wa Shinyanga Asha Kitandala amesema  amefurahi kuona utekelezaji unaenda vizuri Zahanati imepata maji kama zipo changamoto ni ndogondogo zitaenda zikitatuliwa ila wanaipongeza Ruwasa kwa juhudi wanazozifanya kwa miradi ya maji.

Meneja wa Ruwasa wilaya ya Shinyanga mhandisi  Emaeli Nkopi amesema mradi huo umetekelezwa  ndani ya siku 170  na wakandarasi wa ndani ulianza rasmi  tarehe 6,Juni,2023 na 30,Novemba,2023 umekamilka  na umesanifiwa kuhudumia wanachi 2,262 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Nkopi amesema  gharama ya mradi  ni sh  zaidi y ash Milioni 333 na fedha iliyotumika ni zaidi y ash Milioni 159 na  kiasi kilichobaki ni zaidi ya  sh Milioni 173 hivyo amewataka wananchi  wajitokeze kuvuta maji kwa  kwa kuwaona  jumuiya za watumia maji (CBWSO) ambao watawapa utaratibu wa kuijiunga  na fedha zinalipwa kwa njia ya mfumo.

Baadhi ya wananchi waliokuwa  kwenye mkutano ulioongozwa na Mbunge Kirumba walihoji  namna ya taasisi zitakavyolipia ankara za maji na wao kupata maji majumbani ambapo walipata ufafanuzi.


Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga vijijini  akiongea kwenye mkutano wa hadhara kutambulisha wageni.


 Meneja Ruwasa wilaya ya Shinyanga Mhandisi Emaeli Nkopi akisoma taarifa








Mbunge Santiel Kirumba akiongea kwenye mkutano wa hadhara kijiji cha Kilimawe

Viongozi wakiteta  kabla ya kukaribishwa kwenye kikao.

Katibu wa UWT mkoa wa Shinyanga Asha Kitandala akiongea kwenye  mkutano wa hadhara

Mbunge vitimaalum Santiel Kirumba akitoa salamu kwenye mkutano wa hadhara



Wananchi wa kijiji cha  Kilimamawe kata ya Mwantini halmashauri ya wilaya ya Shinyanga

Zahanati ya kijiji cha Kilimawe ikiwa na huduma ya maji

Mbunge Santiel Kirumba akiwa na wanawake wa kijiji cha Kilimawe kata ya Mwantini akishuhudia upatikanaji wa maji.


Wananchi wa kijiji cha  Kilimamawe kata ya Mwantini halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Post a Comment

0 Comments