Header Ads Widget

LIGI YA MPIRA WA MIGUU KAHAMA YAPATA MDHAMINI KWA KUTOA SH MILIONI 40



Mdhamini  aliyetambulishwa na viongozi wa  chama cha mpira wilaya hiyo  Wakili Sweetbert Nkuba akiwakilishwa  na Conrad Nkuba upande wa kushoto akiwa na viongozi wa  mpira wa miguu wilaya hiyo katika ni mwenyekiti Hussein Salum na kutoka kulia ni  katibu  Timoth Fabian

Na  Kareny Masasy,Kahama

LIGI  ya  chama   cha mpira wa miguu wilayani Kahama mkoani Shinyanga (KDFA)  imepata mdhamini   ambaye ametoa sh Milioni 40 kwaajili ya kuendesha ligi hiyo ikiwemo  zawadi za mshindi wa kwanza,pili na watatu, kikombe na medani kwa wachezaji.

Mdhamini  aliyetambulishwa na viongozi wa  chama cha mpira wilaya hiyo  Wakili Sweetbert Nkuba   akiwakilishwa  na Conrad Nkuba amesema atatoa zawadi hizo na yuko tayari kushirikiana na wadhamini wengine.

Mwenyekiti wa chama cha Mpira wa miguu  wilayani hapo   Hussein Salum amesema hayo leo  tarehe 25,Novemba ,2023   mbele ya waandishi wa habari  ambapo ameeleza kupitia fedha hizo mshindi wa kwanza atapata sh Milioni tano na kikombe ,wa pili Milioni tatu na wa tatu sh Milioni moja.

Salum amesema  ligi ya wilaya ina timu kutoka vilabu 21 vya mpira wa miguu  ambavyo vitashiriki  kwenye mchezo wa ligi hiyo  inayotarajia  kuanza kuchezwa tarehe 27,Novemba ,2023 na   timu zitagawanywa kwenye  makundi manne.

“Mdhamini ametoa sh Milioni 40 ambazo zimetumika kuanzia upatikanaji wa jezi,vifaa vingine vya mchezo  na pia atatoa zawadi kwa washindi hao watatu na kiingilio ni bure”amesema Hussein.

Hussein amesema siku ya ufunguzi timu mbili zitapewa nafasi ya kucheza  katika uwanja wa taifa wa wilaya ya Kahama ambazo ni  timu ya  Eagle Sports na Aladini zote za Kahama.

Hussein amesema ligi ya wilaya inatakiwa ichezwe kwa ubora  ambapo wamefanya vikao  na timu zote wakishirikiana na waamuzi  ili mwisho wa ligi kuweza kupata timu iliyobora  kwa kufuata kanuni 17 za mchezo wa mpira wa miguu.

Hussein amesema amfurahi kujitokeza kwa mdhamini huyo ambaye walimuomba  kusaidia ili kuweza kuendesha ligi kwani hali halisi ya vilabu vya timu zilizopo ni duni hazijiwezi kifedha.

 Mwakilishi wa mdhamini wa ligi hiyo Conrad Nkuba  amesema ameguswa kusaidia ligi kuweza kunyanyua vipaji  na kama nafasi ikiwepo ataweza kuongeza zawadi zaidi ya hapo ikiwemo medani  kwa wachezaji  kikubwa ni kuboresha michezo  ndani ya wilaya ya Kahama.

Nkuba amesema yeye hata akijitokeza mdhamini mwingine yuko tayari kushirikiana naye ili kuweza kunyanyua vipaji vya vijana wenye nia ya kutaka kufika mbali.Mdhamini wa ligi ya  mpira wa miguu wilaya ya Kahama  Wakili  Conrad  Nkuba upande wa kushoto akiwa na viongozi wa  mpira wa miguu wilaya hiyo katika ni mwenyekiti Hussein Salum na kutoka kulia ni  katibu  Timoth Fabian

Mdhamini wa ligi ya  mpira wa miguu wilaya ya Kahama  Wakili  Conrad  Nkuba upande wa kushoto akiwa na viongozi wa  mpira wa miguu wilaya hiyo katika ni mwenyekiti Hussein Salum na kutoka kulia ni  katibu  Timoth Fabian



Mdhamini wa ligi ya  mpira wa miguu wilaya ya Kahama  Wakili  Conrad  Nkuba upande wa kushoto akiwa na viongozi wa  mpira wa miguu wilaya hiyo katika ni mwenyekiti Hussein Salum na kutoka kulia ni  katibu  Timoth Fabian



Post a Comment

0 Comments