Header Ads Widget

RUWASA SHINYANGA YAWAFURAHISHA UWT UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI KISHAPU.




Na Kareny Masasy, Kishapu

UMOJA wa wanawake  Tanzania wa chama cha Mapinduzi  (UWT) mkoa wa Shinyanga  umeeleza ukatili uliokuwa unapatikana kwa  wanawake sababu ya ukosefu wa maji safi na salama  Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzaia Samia Suluhu ameuondoa ukatili huo.

Hayo yamesemwa leo tarehe 29,Novemba,2023  na  wajumbe  wa UWT mkoa  wakiongozwa  na  mbunge viti maalum Santiel Kirumba   ambapo amesema  wakala wa  maji safi na  mazingira vijijini (Ruwasa)  mkoa wa Shinyanga wamefanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi ambayo serikali imetoa fedha nyingi.

Kirumba  amesema  kero kubwa ilikuwa ni maji na kipindi cha miakka miwili ya Rais Samia Suluhu ametoa fedha nyingi kwenye miradi ya maji lengo kuondoa kero hiyo kwa wananchi na  waisimamie vizuri kwani miradi inatakiwa kuwa endelevu.

“Mradi huu ni mkubwa  kwa mkoa mzima wa Shinyanga kwa kutumia fedha nyingi  na hatutaki Rais akwamishwe ila tunaipongeza Ruwasa ndani ya mkoa huu haijamkwamisha Rais ipo bega kwa bega”amesema Kirumba.

Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Shinyanga Grace Bizuru amesema    kitu ambacho wamejivunia nikuona wanawake hawateseki tena  na utafutaji wa maji hali ambayo ilikuwa ikiwafanya wapate changamoto ndani ya ndoa zao na wengine kufanyiwa vitendo vya ukatili.

Katibu wa UWT mkoa wa Shinyanga  Aisha Kitandala amesema   lengo la chama kuona wanawake wanatatuliwa kero zao hasa upande wa maji ambao ulikuwa ukionekana ukosefu wa maji ni chanzo cha  ukatili  kwa wanawake nakuwashauri Ruwasa kutumia vibarua wanatoka kwenye eneo hilo ili wanufaike.

Mbunge wa jimbo la Kishapu   Boniface Butondo amesema  ilani ya chama cha Mapinduzi waliyokuwa wakiinadi imetekelezwa vizuri kwa kumtua mama ndoo kichwani kwa vijiji hivyo   kwani kilio kikubwa kwa wananchi wa vijiji hivyo ilikuwa ni kupata huduma ya maji.

Meneja  wa Ruwasa wilaya ya Kishapu  mhandisi Dicksoni Kamazima amesema  ujenzi wa mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Seseko hadi Ngundangali  unagharimu  zaidi ya sh Bilioni 2.8 unatekelezwa na mkandarasi  M/S  na  Otonde Costruction and General Supplier Ltd kwa mkataba  wa mwaka mmoja.

 “Mpaka sasa  tanki la maji linautekelezaji wa asilimia 88.5  na linaujazo wa lita laki moja katika mnara wa mita 15 na kujenga vituo  vya kuchotea maji 31 katika mradi huo”amesema Kamazima.

Wakati huo huo  mhandisi Kamazima amesema  wakazi 49,965 kutoka  vijiji 13 vya kata tatu  vya halmashauri ya wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  watanufaika  na mradi wa maji wa ziwa victoria uliogharimu  zaidi ya sh Bilioni 6.6.

Mhandisi Kamazima  amesema mradi huo unatekelezwa kwa fedha za serikali  na mkandarasi amelipwa malipo ya awali  huku  akivitaja   vijiji vitakavyo nufaika kuwa ni   Igaga A na B, Isagala, Mwamashele, Busongo, Mwamanota, Bubinza, Lwagalalo, Mwamadulu,Nyawa,Beledi,,Lagana na Mihama.

“Utakapokamilika mradi huo  utawapunguzia muda wa kufuata maji umbali mrefu na kuwaongezea muda wa kushiriki shughuli za kiuchumi na kijamii pia kupunguza mlipuko wa magonjwa yatokanayo na kutumia maji yasiyo safi na salama.”amesema Kamazima.

Meneja Ruwasa mkoa wa Shinyanga mhandisi  Juliette Payovela amesema miradi hiyo  ikikamilika itaweza kuwaondolea kero wananchi kwani serikali imeleta fedha za utekelezaji na wakandarasi wapo kazini

 Diwani wa kata ya Lagana  Luhende Sana amesema kata yake ina vijiji vitano ambavyo vyote vitanufaika kwani awali walikuwa wakinunua  maji ndoo  moja sh 1000  au kufuata umbali wa kilomita tano mto tungu.


Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Kishapu Rahel Madundo

Mhandisi Dickson kamazima akitoa maelezo  mbele ya viongozi waliotembelea miradi ya maji.



Mhandisi Dickson  kamazima akitoa maelezo kwa  viongozi wa UWT waliotembelea mradi wa maji





Asha Katandala ambaye ni katibu wa UWT mkoa wa Shinyanga akiwatambulisha viongozi wenzake


Mhandisi  wa Ruwasa mkoa wa Shinyanga Juliette Payovela akiwa na mbunge viti maalum  Santiel Chilumba  kwenye mradi wa maji


Mbunge viti maalum Santiel Chilumba akipiga makofi kwa Ruwasa baada ya kufanya vizuri kwenye miradi

Tanki la maji lililopo kwenye kijiji cha Lagana wilayani Kishapu

Post a Comment

0 Comments