Header Ads Widget

RUWASA YAWAPA RAHA VIONGOZI SHINYANGA MRADI WA MAJI MASENGWA VITUO VYA KUCHOTEA MAJI 46



 WAKALA wa maji safi na mazingira vijijini (Ruwasa)  wilaya ya Shinyanga  imekamilisha  mradi wa maji  Masengwa.

Na Kareny Masasy,Shinyanga

WAKALA wa maji safi na mazingira vijijini (Ruwasa)  wilaya ya Shinyanga imeeleza ukamilishaji wa mradi wa maji  Masengwa  ya awamu ya pili kwa viongozi wa umoja wa wanawake Tanzania (UWT) wa Chama cha Mapinduzi  wa mkoa Shinyanga.

Meneja wa Ruwasa Mhandisi  Emael Nkopi amesema hayo jana tarehe 30,Novemba,2023  mbele ya viongozi hao ambao walikuwa wakiongozwa na Mbunge Santiel Kirumba  katika  kutembelea miradi ya maji iliyotolewa fedha na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Mhandisi Nkopi amesema ujenzi wa tanki la maji ishinabulandi umekamilika na linatoa huduma katika vijiji viwili vya Ishinabulandi na Bubale ikiwa tanki linaujazo wa lita 200,000 nalimekamilika.

Kuna vituo 46 vya kuchotea vimejengwa katika maeneo tofauti,vituo 15 vya Bubale na Ishinabulandi vnatoa huduma ya maji na vituo nane vya Isela,Idodoma,vinatoa huduma ya maji na vituo nane vya  Ibingo na Ngwa’nghalanga viko kwenye majaribio na muda sio mrefu vitaanza kutoa huduma ya maji.

Mbunge Santiel Kirumba alipongea kwa kazi hiyo ambayo wananchi wengi sasa wanapata maji safi na salama hivyo  waziri wa maji Juma Aweso na  Wahandisi wa  maji mkoa wa Shinyanga mungu awabariki kwa kazi nzuri yenye uaminifu kwani ukosefu wa maji  umeanza kuwa historia.

“Mhandisi wa maji ni mwanake ambaye ni Juliette Payovela ameguswa kwelikweli na wanawake kumtua ndoo kichwani ametekeleza kwa vitendo  kazi yake anayopaswa kuifanya kwa kusimamia fedha na  anastahili kupongezwa ukatili wa wanawake kupitia maji sasa basi…”amesema mbunge Kirumba.

Katibu wa UWT mkoa wa Shinyanga Asha Kitandala amesema  kazi nzuri imetekelezwa na serikali na ilani ya chama cha Mapinduzi imeenda vizuri wananchi  wa maeneo ya vijiji na kwenye baadhi ya shule zinapata maji.

“Rais wetu  Samia Suluhu Hassan mungu amubariki kazi amefanya kwa vitendo tunajionea tumepita kila maeneo yenye mradi wa maji imerizisha kweye utekelezaji na imekamilika”amesema Kitandala.

Mbunge  vitimaalum Santiel Kirumba akifungua maji moja ya kituo cha kuchotea maji kilichopo shule ya msingi Masengwa.
Mbunge vitimaalum Santiel Kirumba akiongea na wanafunzi wa shule ya msingi Masengwa.

Tanki la maji  lilojengwa  nakusambaza maji kwenye vituo vya kuchotea maji.

Viongozi wakifurahishwa na utendaji wa Ruwasa mkoa wa Shinyanga.



Post a Comment

0 Comments