Header Ads Widget

TRA KAHAMA YATOA SHUKRANI KWA KUWAONA WAGONJWA NA KUKABIDHI MAGODORO WODINI





Mmoja wa wafanyakazi wa TRA  akimuona mgonjwa wodini.

  Na Kareny Masasy,Kahama

MAMLAKA  ya Mapato  Tanzania (TRA) mkoa wa Kikodi Kahama, umekabidhi msaada wa Vifaa mbalimbali katika Hospitali ya Manispaa ya Kahama kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa Jamii ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Shukran kwa Mlipa Kodi.

Akizungumza  hayo leo tarehe 1/Desemba/2023 mara baada ya kukabidhi msaada huo Mwakilishi wa meneja kutoka mkoa wa Kikodi Kahama, Wisaka Kamwamu amesema kuwa msaada huu ni  sehemu ya kutambua mchango unaotolewa na Jamii.

Kamwamu akikabidhi msaada huo amesema  TRA itaendelea kufanya hivyo katika Maeneo mengine kwa shukrani ambayo wameendelea kushirikiana na jamii.

Akipokea Msaada huo kwa niaba ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Manispaa ya Kahama, Dk Allan Masanja ameishukuru  TRA  kwa Msaada huo.

 Ikiwa  wametoa  Magodoro ambayo ameeleza  yatakwenda  kusaidia maeneo muhimu  kutokana na hospitali hiyo kuwa na idadi  ya  wagonjwa  wengi kulazwa na wanaohudumiwa

Masanja amewataka  wadau wengine kujitokeza kutoa msaada kwa ajili ya wenye uhitaji.

Vifaa vilivyokabidhiwa leo ni pamoja na Magodoro 30, Juice, Maji, Miswaki na vitu vidogo tofauti kwa wagonjwa waliokuwa wamelazwa katika wodi tofauti tofauti.

Wafanyakazi wa TRA  mkoa wa kikodi Kahama










Post a Comment

0 Comments