Header Ads Widget

PJT-MMMAM YATAMBULISHWA KWA WATAALAMU NA VIONGOZI WA DINI HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU.



   DC- Kishapu akiwa na  wataalamu na viongozi wa dini

 Na Kareny Masasy,

OFISI  ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na Shirika la ICS imetoa utambulisho wa namna ya utekelezaji wa mpango wa Jumuishi wa Taifa  Makuzi,Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto   (PJT MMMAM) kwa viomgozi na wataalamu wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kishapu ili waweze kuwafikisha watoto kwenye ukuaji timilifu.

 Akiwasilisha programu hiyo  leo  Afisa  ustawi wa jamii   kutoka mkoani Shinyanga Lyidia Kwesigabo  alisema  ili mtoto aweze kufikia hali nzuri ya ukuaji bado ni lazima  kusimamiwa kwenye nguzo tano  ambazo ni Afya,Lishe bora, Ujifunzaji wa awali,Malezi yenye mwitikio na ulinzi na Usalama.


Kikao hicho kiliratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la  investing in Children and Strengtherning  their Societies (ICS) nakuhudhuriwa na viongozi pamoja na wataalamu wa idara mbalimbali ambapo  Lydia Kwesigabo alisema jamii inatakiwa ipate elimu hii muhimu kwa ujumuishi wake kwa faida ya watoto familia na Taifa kwa ujumla.
 
Kwesigabo amesema programu hiyo ilizinduliwa mwezi Desemba 2021 na ni programu ya miaka mitano 2021/2022  hadi 2025/2026  ambayo imelenga watoto kuanzia umri wa mwaka  0 hadi miaka ( 8) ambao ni umri  uko katika hatua ya ukuaji.
 
“Kwesigabo  amesema  kuhusu dhana za ujifunzaji zinaweza kuandalliwa kulingana na mazingira huskika kwa kutumia vitu vya asili na zikatumika katika vituo vya Kulelea watoto wadogo mchana na shule za awali.
  
Kwesigabo amesema  nguzo zote 5 ni  muhimu kwa watoto na pia  mama anapokuwa mjamzito hatakiwi kuwa na msongo wa mawazo na pia baba na mama wanatakiwa wamsemeshe mtoto aliyeko tumboni  kwani pia husaidia mtoto kukua tumboni akiwa na furaha na uchangamshi mzuri na Ubungo kuendelea kukua vizuri
Mgeni rasmi ambaye ni  Mkuu  wa wilaya  ya Kishapu Joseph Mkude amesema programu hiyo ataisimamia vizuri hata kwenye ngazi za vijiji na kata kuhakikisha watoto wanakuwa katika mazingira Bora.
 
"Kuna baraza la madiwani kesho kutwa nitazungumza programu hiyo kwa madiwani ili waweze kuuelewa na hakuna kitakacho shindikana  watumia rasilimali zilizopo kwenye maeneo Kama alivyosema  afisa ustawi wa jamii"amesema Mkude.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Emanuel Jonson amesema  programu hiyo imekuja wameipokea watatekeleza huku sheikhe  kutoka Kishapu  Adamu Nkhambi alisema wanaume wanafikiri wakiweka ujauzito inatosha kumbe Kuna Malezi zaidi yanahitajika ili mtoto aweze kukua vizuri na mwenye maadili.
Mwenyezi Mungu  katika vitabu  vyake  amesema kazaeni mjaze dunia tafsiri yake  kwenye Malezi  wanaume  na wanawake wawajibike  utakuta mama anaenda mwenyewe kliniki wakati wa ujauzito hadi  anajifungua ,Malezi ya watoto yukoi peke yake  hivyo kama Viongozi wa Dini wataendelea kuelimisha waumini wao juu ya programu hii

Mkuu  wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akishika toleo la kitabu cha  PJT-MMMAM.



Mkuu wa wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Joseph Mkude  akisikiliza utambulisho wa  PJT-MMMAM

Sheikhe   Adamu Nkhambi kutoka kishapu akichangia mada kuhusu PJT-MMMAM


Mkuu wa wilaya akiwa na viongozi wa dini.




Post a Comment

0 Comments