Header Ads Widget

WATAALAMU WA MANISPAA SHINYANGA WAAHIDI KUTEKELEZA PROGRAMU PJT-MMMAM KIKAMILIFU



Makundi mbalimbali na Wataalamu wa Manispaa Shinyanga

Na Kareny Masasy,Shinyanga

WATAALAMU  wa Manispaa ya Shinyanga  wameiahidi  timu ya mkoa  wakishirikiana na  shirika lisilo la kiserikali la  Investing in Children  and Strengthening  their societies (ICS) juu ya utekelezaji wa Programu jumuishi ya taifa ya Makuzi ,Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto( PJT-MMMAM).

Ambapo leo program hiyo imezinduliwa kwa Manispaa  hiyo  nakuhudhuriwa na makundi mbalimbali ikiwemo  baadhi ya  mashirika yanayotekeleza miradi ya afya  na  jamii huku mwezeshaji ambaye ni mratibu  wa Elimu ya afya  kwa umma mkoa Moses Mwita  alitoa elimu juu ya nguzo tano zinazo mfanya mtoto kuwa katika ukuaji timilifu.

Naye Mratibu wa PJT MMMAM Mkoa Lydia Kwesigabo  aliwapitisha washiriki juu ya mwongozo wa uratibu pamoja na viashiria ambabyo Halmashauri na Mkoa watakuwa wakipimwa navyo 

Naye Afisa Mradi toka Shirika la ICS Lucy Maganga alieleza kuwa shirika linashughulika na masuala ya malezi katika mkoa litahakikisha linashirikiana na Mkoa pamoja na halmashauri na wadau wengine katika kuhakikisha lengo la PJT MMMAM linafikiwa 

Ofisa Lishe manispaa ya Shinyanga Amran  Mwakipesile amesema  program hii imekuwa jumuishi hivyo wataitekeleza kwa ushirikiano huku Kaimu mganga mkuu wa Manispaa Charles Malogi akisema watahakikisha wanaifanya vizuri kwenye upande wa afya na ustawi wa jamii kupitia afua mbalimbali.

Mratibu wa chanjo manispaa ya Shinyanga Ramadhani Maneno amesema  wao watatekeleza program hiyo  sababu mara nyingi wamekuwa wakishughulika na watoto kuboresha afya zao kwa kupata chanjo za aina mbalimbali.

Mwenyekiti wa baraza la ushauri  la Manispaa ya Shinyanga Stepheno  Tano  amesema program hiyo wameipokea huku akiahidi  katika utendaji kazi kupitia baraza  la wazee wataitambulisha PJT-MMMAM Ili  wengine waweze kuifahamu zaidi.

Katibu wa bakwata wilaya ya Shinyanga Ramadhani Majani  na Mwinjilisi wa  kutoka kanisa la KKKT  Kanoni Ndembezi  Josephat   wamesema program hiyo wataipeleka kwenye makundi waliyonayo yanayotoa elimu ya Malezi  kwa wanawake na wanaume ili waifahamu na kutekeleza yanayowahusu kwa watoto.

Mwita  amesema  nguzo hizo zinatambuliwa kuwa ni  Malezi yenye Mwitikio,lishe bora,afya, Ujifunzaji wa awali pamoja na Ulinzi na Usalama  akielezea  suala la lishe anasema mama mjamzito anatakiwa  apate lishe iliyobora katika siku 1000  ili kumuweka mtoto katika afya nzuri.


“Ndiyo maana serikali inasisitiza  halmashauri kutenga shilingi 1000 kwaajili ya lishe kwa mtoto baada ya kuona ipo changamoto kwenye jamii”anasema Mwita.

Mwita  amesema wengi wamekuwa  hawafahamu  kuwa baba  anatakiwa kuweka  malezi yenye mwitikio  kwa watoto wasiwaache  kina mama peke yao na programu hiyo imelenga watoto kuanzia umri 0 hadi miaka nane.

Mratibu wa program  hiyo mkoa  ambaye ni ofisa  Ustawi wa jamii  Lyidia Kwesigabo amesisitiza suala la kuweka bajeti na mipango ya kila mwaka kwankuanzia na mwaka wa fedha 2024/25 shughuli za PJT MMMAM kwa sekta zote zinazo shughulika na mtoto.

Aidha Alisisitiza ujumuishaji wa agenda ya MMMAM katika vikao vya kisekta,Kamati za kudumu, vikao vya WDC na Baraza la madiwani




Post a Comment

0 Comments