Header Ads Widget

WILAYA YA KAHAMA YAPOKEA PROGRAMU JUMUISHI YA MMMAM WATAALAMU WAAHIDI



Mkuu wa wilaya Mboni Mhita akielezea PJT-MMMAM

Na  Kareny  Masasy

 SERIKALI ya mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na shirika lisilokuwa la kiserikali la  (ICS)  limefanikisha katika uzinduzi wa programu  jumuishi ya Taifa ya Malezi,Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto   (PJT-MMMAM ) katika halmashauri tatu za wilaya ya Kahama.

Halmashauri hizo ni  Msalala,Ushetu na manispaa ya Kahama ambapo uzinduzi huo umefanyika kwa kila halmashauri huku mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita akifungua  rasmi program hiyo  leo huku wakurugenzi wakipokea na kuahidi kushirikiana katika utekelezaji.

Mboni amesema  programu  hiyo imekuwa shirikishi ambapo imekuja kutatua changamoto na kuboresha huduma za Malezi ya watoto  kwa kuwa na nguzo tano muhimu zilizoainishwa  hivyo   program hii itatoa uelewa mpana na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha inasonga  mbele.

Mkurugenzi wa halmashauri ya Ushetu Hadija Kabojola amesema yeye ni mama nani mlezi anafahamu umuhimu wa program hiyo ambayo inakwenda kumjenga mtoto ikisimamiwa vizuri kwa ujumuishi ulivyo.

Mratibu wa Elimu ya afya kwa Umma Mkoa Moses Mwita  ambaye alikuwa mwezeshaji amesema  suala la ulinzi na usalama,ujifunzaji wa awali na malezi yenye mwitikio mfano mtoto anaposikia sauti ya kufokewa anajua au mtoto akiwa ananyonyeshwa huku mama akiwa hamjali inshara atakayo muonyesha ni kumng’ata.

 zaidi kwa wazazi na jamii inayowazunguka  wazazi wamekuwa hawashangai kuona watoto wao wakiwa wadogo kuzurura mtaa wapili bila kuwa na muangalizi.

Mratibu wa afya ya uzazi,mama,baba na mtoto mkoani Shinyanga  Halima Hamis ambaye alikuwa mwezeshaji kuhusu program hiyo amesema  kupitia sayansi  ya elimu ya makuzi (SECD) inaonyesha mtoto  anazaliwa akiwa na uelewa na kadri anavyokuwa ndivyo  anavyoingiza kila kitu katika ubongo wake.

“Tusifanye vitu kwa kusema huyu ni mtoto haelewi au kuongea lugha zisizo faa mbele yao ndivyo anavyo nasa kwa kuona na kujifunza  na kadri anavyokuwa katika ubongo wake unanasa”anasema Halima.

Afisa ustawi wa jamii mkoa Lyidia Kwesigabo  amesema program hii imekuja kuinarisha uratibu na mashirikiano katika kufanya kazi kwa ujumuishi na ushirikiano, aidha alieleza juu ya viashiria ambabyo kila halamshaui mpk mkoa utapimwa navyo  hivyo ni jitihada zinatakiwa kila mmoja katika eneo lake kuhakiksha anatekeleza programy hii na elimu hii kuishusha kwenye ngazi za kata na vijiji au vitongoji ili jamii iweze kufikiwa.

Afisa Elimu ya Watu Wazima Dedan   Rutazka amesema  mtoto anapoanzia tumboni hadi miaka minane anatakiwa apate lishe ya kutosha ili hata mtoto akiwa  darasani apate uelewa wa kutosha  huku Mratibu wa mradi wa Boost  Fausta Luoga amesema mwanafunzi anatakiwa apate chakula shuleni wazazi wahamasishwe wachangie na walimu wapande mbogamboga shuleni.

Mganga mkuu kutoka halmashauri ya Msalala  Sisti Mosha amesema yote yaliyozungumzwa kwenye program hiyo watakwenda kuyafanyia kazi  hasa kupia kwenye idara ya afya, ustawi wa jamii na lishe

Mchungaji Mapambano Sakobo pia mkurugenzi wa House of Hope   kutoka  Nyangalata Msalala amesema program hiyo imekuja na mambo mtambuka ambayo mengine yanaweza kutatuliwa na kutoa elimu zaidi kwa wazazi ili watoto wapate malezi mazuri yanayotarajiwa.

Ofisa mipango kutoka halmashauri ya Ushetu Shigela  Ganja   nimefurahi kwa kuunganishwa program hii ingependa maelekezo yatolewe namna ya ulaji zipatikane mbogamboga shuleni ili kuelekeza kwenye lishe kwani ubongo wa mtoto kwenye miaka 0 hadi minane inakuwa kwenye hatua  ukuaji.

Mkuu wa kitengo cha sheria  kutoka Manispaa ya Kahama Stephen Magalla amesema zimesemwa changamoto nyingi kwa watoto ambapo ipo sheria ya mtoto  namba 21 ya mwaka 2009 ambayo inatumika ni kuhakikisha inasimamiwa vizuri ili kuwaokoa watoto nay ale yote yaliyoelezwa yatasimamiwa.

Lucy Magnga kutoka shirika la ICS amewaeleza  wataalamu,viongozi wa dini na makundi  ya kijamii kuwa wao kuungana na serikali ni kutokana na shirika hilo kushughulikia masuala ya malezi ya watoto  nakuwataka kushiriki vyema programu hiyo ili kumkomboa mtoto





Post a Comment

0 Comments