Header Ads Widget

MADIWANI USHETU WAWEKA MIKAKATI YA KUPATA HATI SAFI KILA MWAKA



Mwenyekiti wa halmashauri ya Ushetu Gagi Lala akifungua kikao

Na Kareny Masasy,Ushetu

HALMASHAURI  ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga imepata hati safi  ambayo wameeleza inatakiwa waipate kila mwaka huku ukusanyaji wa mapato kwa vipindi vya robo ya pili na robo ya tatu vikienda vizuri.

Katika  kikao cha  baraza la Madiwani  cha  robo ya tatu ya mwaka  kilichofanyika leo tarehe 23,Mei 2024  ambapo madiwani walipitia ajenda ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ukusanyaji wa mapato  ambapo robo ya pili walifikia ukusanyaji kwa asilimia 104 na  robo ya tatu  wako hatua nzuri ya kupita lengo.

Diwani wa kata ya Kinamapula Samweli Sharifu amesema  usimamizi wa ukusanyaji mapato umekwenda vizuri  ukilinganisha na mwaka wa fedha  2021/2022 ambao  ukusanyaji ulikuwa mbovu na kuwasababishia kupata hati chafu.

“Vikao vya baraza la madiwani kwa mwaka ambao walipata hati chafu kila mmoja alikuwa akitafuta  nani kasababisha  na majadiliano yalikuwa makali baadaye walipata suluhisho nini kifanyike ili kuinusuru halmashauri hii”amesema Sharifu.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Ushetu Gagi Lala amesema kweli  lakini hawakukata tamaa walijipanga na kuweka mikakati  ya kusonga mbele na sasa wamevuka vizuri kwa ushirikiano na miradi inatekelezwa.

 Mwakilishi kutoka ofisi ya katibu tawala mkoa wa Shinyanga  Ibrahimu Makana amewapongeza madiwani na wataalamu kwa ushirikiano ambao wanauonyesha nakufikia kupata hati safi na wajitahidi kufuta hoja zinapoibuka.

Aidha taasisi mbalimbali za serikali ziliwasilisha taarifa zao ambapo wakala wa barabara mjini na vijini (Tarura) walieleza kuanza kuzifanyia kazi barabara zilizoharibiwa na mvua  kwa fedha za dharura na zile ambazo zipo kwenye mpango wa bajeti.




Post a Comment

0 Comments