Header Ads Widget

VIFO VYA WATOTO WACHANGA VIMEPUNGUA MANISPAA KAHAMA


  Jengo la  Hosptali ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga.

Na Kareny  Masasy,

UKWELI  usio pingika hakuna mwanamke ambaye ana beba ujauzito na ikifikisha  miezi tisa anapojifungua  akose  mtoto kwani  matarajio yake  ni kupata mtoto mwenye afya njema na kuendelea kuishi.

Baadhi ya wanawake Manispaa ya  Kahama  Maimuna Deus na Blandina Haule wanasema  watoto wanaofariki mara nyingi wazazi wamekuwa wakielezwa amekunywa maji ya tumboni au  kashindwa kupumua.

“Mimi nilifiwa na mtoto mchanga hakufikisha siku 28 kwanza hakulia wakati namzaa walimpiga piga mgongoni  ili ashtuke na baadaye akalia lakini tulikwenda nyumbani wakawa wananiambia ana  ugonjwa wa degedege”anasema Haule.

 

Mratibu wa afya ya  Uzazi  Mama na mtoto Manispaa ya Kahama  Caroline Malesela anasema kupitia mradi wa Saver bandle of  birth Care (SBBC)    ulioanza mwaka 2021 mwezi Februari kwa  kutoa mafunzo kwa watoa huduma  56  nao wakawa  vinara wa kuwafundisha wenzao.

“Mradi pia umeleta  vifaa kwaajili ya kujifunza  na  vifaa vya kumpima mtoto  ili kuona mapigo ya moyo kwa mtoto  kama yupo hai   zamani utaalamu na vifaa hivyo hatukuwa  nao na watoto walikuwa wanapoteza maisha” anasema Malesela.

Malesela anasema  Manispaa ya Kahama  Vituo sita  vimepata  wahudumu   waliopitia mafunzo na kupitia mradi  huu  wadau hao wameajiri watu wanaofuatilia   takwimu  za  mama wanaojifungua  salama pamoja na watoto  na waliopoteza maisha pia .

“Takribani   kwa siku watoto wanazaliwa  kwa hospitali ya manispaa ya Kahama ni  35 hadi 40  na  kwa mwezi watoto zaidi ya 1000 na kila mtoto anaweza kuzaliwa na changamoto zake”anasema Malesela.

Watoto wengi wametambulika na kupona  ndiyo maana tulikuwa tunaendelea kuona vifo vya watoto wachanga vinazidi ikiwa mwaka 2020 kulikuwa na vifo  382 vya watoto wachanga.

Baada ya mradi kuanza   waliona mabadiliko ya kuokoa vifo hivyo  mpaka  mwezi Desemba 2021  kulikuwa na vifo  vya watoto wachanga 350  na mwaka 2022 kulikuwa na vifo 326 na mwaka 2023 kulikuwa na vifo 281.

Muuguzi kinara kutoka ofisi  ya  Muuguzi kitengo  cha  kujifungua  Zahara Hassan anaelezea namna wanavyofanya kazi ya kumuokoa mtoto baada ya kuzaliwa  kupitia mradi wa kitita cha uzazi salama ambao umesaidia kuokoa vifo vya watoto wachanga kwa asilimia kubwa  wilaya nzima ya Kahama.

Hassan anasema baada ya kupata mafunzo  amekuwa wakitembea kwenye wodi ya kujifungua  kutoa elimu kwa wengine namna ya kumuhudumia mtoto mwenye shida ya kupumua ambapo imekuwa ikitokea kwa baadhi ya watoto na kuokoa maisha yao.

“Tumepewa vifaa maalum na kupata mafunzo ya  namna ya kutumika   kifaa cha kupima mapigo ya moyo na kifaa cha kuweka tumboni baada ya mtoto kuzaliwa”  anasema Hassan.

Hassan anasema kulingana na takwimu za vifo vya watoto wachanga wengi walikuwa wakifariki  wakiwa bado tumboni na wengine wenye siku moja hadi 28 kutokana na hali ya kutopumua vizuri na kukosekana utaalamu kwa watoa huduma.

Muuguzi Nyabiseko Kadidi kutoka Kitengo cha uangalizi wa  watoto wachanga  Manispaa ya Kahama anasema wapo  watoto wenye  matatizo  mbalimbali  ambapo wamekuwa wakilazwa kwa siku watoto  kumi  hadi 15   na ndani ya mwezi takribani watoto 150 hadi 80.

Mkurugenzi wa Afya,ustawi wa jamii na Lishe kutoka ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za Mitaa   Dk Rashid Mafume anasema zipo jitihada zimefanyika  kwenye mradi wa   Kitita cha uzazi salama ambacho  kimesaidi  upatikanaji wa kifaa kinachoitwa Moyo kupima mapigo ya mtoto na  kifaa kinachoitwa Nevit  kupima tumboni kwa mama.

“Hali ilivyo sasa nchini kumeanza kupungua  vifo vya watoto wachanga kutokana na  teknolojia  iliyotumika ya kuwa na  vifaa vya upimaji,matumizi ya takwimu na mafunzo kwa watoa huduma”anasema Dk Mfaume.

Dk Mfaume anasema vifo vya watoto wachanga hali ni mbaya  walichobaini  wataalamu walikuwa wanahangaika kupata mapigo ya moyo ya mtoto  vifaa vilikuwa havipo  na walipokuwa wakiona mtoto asipo hema  wanamhesabu amefariki lakini sasa watoto wengi wameokolewa.

 vifo vya watoto wachanga nchini vimepungua kwa asilimia 25 ni suala la kuwapongeza wadau  na wataalamu wanao shauriana kwani wakilenga  kuokoa vifo vya mama watakuwa pia wanapunguza vifo vya watoto wachanga na  kupanua wigo  wa mafunzo  wa wauguzi kwenye vituo vyote.

Dk Mfaume anasema Shughuli nyingi zilikuwa zinafanywa na wadau kuhusu kupunguza vifo vya wajawazito nakusahau kuokoa maisha ya watoto wachanga na sasa kupitia mpango huu  inawasaidia watoto kuwaangalia wakiwa bado tumboni na mpaka anazaliwa.

Mratibu wa mradi wa  kitita  cha uzazi Salama (SBBC)  mkoa wa Shinyanga Janeth Mpemba unajihusisha na  uzazi salama,  mama wanaofariki wakati wa kujifungua  na vifo vya watoto wachanga na watoto njiti.

“Tulianza mradi huu mwaka 2021 kwa mkoa  huu   kipindi cha   miaka mitatu  tulikuwa na malengo matatu kupunguza vifo vya  mama kwa asilimia kumi ,watoto wachanga  kwa asilimia 50”anasema Mpemba.

Mpemba  anasema  kipindi cha mradi awamu ya kwanza ilikuwa  ni utafiti wakagundua vifo vya watoto wachanga vinachangiwa na watoa huduma  kutojiamini  na sasa wamewekeza kutoa mafunzo  na vifaa ambapo vimepunguza vifo vya watoto wachanga.

Mpemba anasema mkoa wa Shinyanga walianza  kwenye  vituo sita na kipindi cha pili cha mradi wameongeza vituo nakufikia   28 na wahudumu 56 wamekwisha patiwa mafunzo.

Sera ya afya ya mwaka 2007 imewekeza katika kuboresha  uhai wa mtoto kupitia utoaji wa huduma za afya bure kwa kina mama wajawazito  na watoto chini ya miaka mitano.

Uwekezaji wa serikali katika uhai wa mtoto unaonekana dhahiri kwenye kupungua kwa vifo vya watoto kati ya mwaka 2010 hadi 2015 ambapo kiwango cha vifo vya watoto wachanga  kuanzia siku 0 hadi 28 vimepungua  kutoka vifo 40 hadi vifo 25 kwa kila kizazi hai 1000.

mwisho

 


Post a Comment

0 Comments