Header Ads Widget

DC MTATIRO AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI ILANI YA CCM KWA HALMASHAURI KUU YA CCM WILAYA YA SHINYANGA MJINI

DC MTATIRO AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI ILANI YA CCM KWA HALMASHAURI KUU YA CCM WILAYA YA SHINYANGA MJINI

Na Marco Maduhu,SHINYANGA

DC Mtatiro.

MKUU wa Wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro,amewasilisha Taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, ya mwaka 2020/2025 kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Juni 2024.

Amewasilisha taarifa hiyo leo Juni 20,2024 kwenye Kikao Maalum Cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini.

Amesema kwa kipindi hicho Rais Samia ametoa fedha nyingi Zaidi ya Bilioni 35.6, ambazo zimetekeleza Miradi mbalimbali ya Maendeleo kwa wananchi. na kuitekelezaji Ilani ya CCM kwa asilimia 100.

Uwezeshaji wananchi kiuchumi

Akielezea eneo la Uwezashaji wananchi kiuchumi, amesema Serikali chini ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, imeendelea kutoa fedha kwa Walengwa wa TASAF na kuzinusuru Kaya Maskini, pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa kurudisha Mikopo ya Halmashauri asilimia 10.

Miundombinu ya Barabara

Amesema Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA)Tayari wameshapokea kiasi cha fedha Sh.Milioni 853 kwa ajili ya uboreshaji wa Miundombinu ya barabara.

“Hapa kwenye Barabara napenda kuzungumza kidogo kuna Miradi 10 ambayo inaendelea ya ujenzi wa Barabara, lakini iliyokamilika ni Miradi 4, na Miradi 6 bado haijakamilika, na Miradi hii 6 ipo ndani ya uwezo wangu, Wakandarasi wajipange wapo ambao tutavunja Mikataba, kuwakamata,na kuzuia wasifanye kazi tena hapa Shinyanga,”amesema Mtatiro.

Maji

Amesema kwa maeneo ambayo bado hajafikiwa na huduma ya Maji, Mikataba mbalimbali imesainiwa na wapata pata huduma hiyo.

Umeme

Amesema kazi ya kusambaza ya umeme inaendelea na wananchi wengi wameshafikiwa na huduma hiyo.

Afya.

Amesema huduma za Afya zinaendelea kuboreshwa na Rais Samia, na hivi karibuni ametoa fedha katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga Zaidi ya Sh.bilioni 1, na ukarabati wa Majengo unaendelea.

 “Rais Samia pamoja na wasaidizi wake akiwamo na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi,amekuwa wakifanya kazi kubwa sana kwenye Sekta ya Afya, tunaona mambo makubwa ambayo yanafanyika, tuendee kuwa unga mkono na kuwatia Moyo hawa viongozi wetu,”amesema Mtatiro.

Elimu

Amesema fedha zimeendelea kutolewa kwenye Sekta ya Elimu, zikiwamo za Elimu bure, pamoja na kuboresha miundombinu ya Sekta hiyo zikiwamo Maabara za Sayansi na wanafunzi wanasoma katika mazingira rafiki.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anorld Makombe, akizungumza kwenye kikao hicho,amempongeza Rais Samia kwa kuitekeleza ilani ya CCM kwa asilimia 100 na kufanya mambo makubwa ya kimaendeleo ikiwamo ya kimkakati.

Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo naye ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Samia, pamoja na wasaidizi wake kwa kazi kubwa ambayo anaifanya, wakiwamo na Watumishi wa Serikali kwa kusimamia miradi ya maendeleo vizuri na kuzitendea haki fedha ambazo zinatolewa na Rais.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akiwasilisha Taarifa ya Ilani ya CCM kwa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akiendelea kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Ilani ya CCM 2020/2025.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Anorld Makombe akizungumza kwenye kikao hicho.
Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Sharifa Mdee akizungumza kwenye kikao hicho.
Katibu wa Siasa,Uenezi na Mafunzo CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Said Bwanga akizungumza kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Alexius Kagunze akijibu maswali kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Alexius Kagunze akiendelea kujibu maswali kwenye kikao hicho.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Wakuu wa Idara halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye kikao hicho.
Wakuu wa Idara halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye kikao hicho.
Wakuu wa Idara halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye kikao hicho.

Post a Comment

0 Comments