Header Ads Widget

DC MKUDE AWATAKA WANANCHI KISHAPU KUSHIRIKI KIKAMILIFU ZOEZI UANDIKISHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA


Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura pamoja na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mhe. Mkude amebainisha hayo jana alipokuwa akifunga Mashindano ya Mpira ligi ya kata ya Ukenyenge

"Ninashukuru sana kwa kunialika kuja kufunga Mashindano haya ya ligi ya Kata ya Kunyenge kwa kuwa mimi ni Mwanamichezo ninayofuraha sana kuzipongeza timu zilizoingia Fainali timu ya Bulimba na Timu ya Wila ninawatakia Mchezo Mwema wenye ushindani mzuri, Pia nitumie fursa hii Kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa Wingi pindi utakapoanza Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura na kushiriki kimalifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kwani ni haki ya kila mtu kumchagua kiongozi anayeona anafaa. Alisema Mkude.

Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Ukenyenge Mhe. Underson Mandia amezipongeza timu zote zilizofika fainaili kwani mashindano hayo waliyaanzisha kwa lengo la kuhamasisha Wananchi kuutambua Mchakato wa Uchaguzi ili waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi Uchaguzi 2024.

Naye Katibu Tarafa wa Kata ya Negezi Bw, Omary Mwenda amesema mashindano hayo yana tija kubwa Sana katika kuhamasisha wanachi kushiriki kikamilifu katika uandikishaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na kuahidi kufanya mashindano hayo kila kata ndani ya Tarafa ya Negezi

Aidha katika Mashindano hayo timu ya Wila iliibuka Mshindi kwa kuiadhibu timu ya Bulimba gori moja ambalo lilifungwa na Mshambuliaji Anthony Masunga.

Post a Comment

0 Comments