Home
About
Contact
Header Ads Widget
HOME
SHINYANGA
HABARI
MAGAZETI
SIASA
MATUKIO
AFYA
MICHEZO
Home
habari
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Maduhu
June 28, 2024
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Na. Paul Kasembo, KAHAMA MC.
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka watalaam wakiongozwa na Wakurugenzi wao kubadilika na kuanza kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) ili waweze kuzipunguza kama siyo kuziondoa hoja zote badala ya kusubiria wakati wa ukaguzi ili waanze kupambana kujibu wakati nafasi ilikuwepo ya kufanya hivyo awali.
RC Macha ameyasema haya leo tarehe 28 Juni, 2024 alipokuwa akifunga mkutano maalum wa baraza la madiwani katika Manispaa ya Kahama ikiwa ni hitimisho la mikutano maalum ya CAG kwa Halmashauri zote sita (6) zinazounda Mkoa wa Shinyanga huku akisisitiza umuhimu wa waheshimiwa madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kwa wananchi wao ili waweze kuaminika na kupata hati safi za vipimo vya wananchi na wapate ridhaa tena ya kuongoza ukizingatia kuwa wananchi nao wanayo nafasi ya kupimwa kwa wananchi wao.
"Niwashauri sana wataalam wetu mkiongozwa na wakurugenzi wenu mbadilike na muanze kushirikiana kwa kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya CAG ili itakapofika wakati wa ukaguzi muweze kuziondoa kama siyo kuzifuta hoja zote badala ya kusubiria ufike muda wa ukaguzi ndiyo muanze kupambana kuziondoa wakati mlikuwa na hiyo nafasi kufanya kazi pamoja na kushirikiana," amesema RC Macha.
Aidha RC Macha ameitaka Manispaa ya Kahama kuhakikisha wanavipata vikundi vyote vioivyotajwa kuwa havionekani baada ya kukopa fedha kutoka kwenye mfuko wa asilimia 10 ambapo wanawake 4%, vijana 4% na watu wenye ulemavu 2% ili waweze kuzirejesha pamoja na kujibu hoja ya CAG inayotokana na madeni hayo.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya CAG kwa 2022/2023 Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu ndg. Godwin Dinda kwa niaba ya Mkurugenzi ndg. Masudi Kibeto amesema kuwa Manispaa ya Kahama ilikuwa na hoja 25 ambapo hoja 9 zimejibiwa na kufungwa, huku 12 zikiwa kwenye utekelezaji, hoja 3 hazijatekelezwa na hoja 1 imejirudia.
Akiahirisha baraza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kahama Mhe. Yahaya Bundala amesema kuwa wamepokea pongezi zote kwa kupata hati safi mfululizo, wamepokea maelekezo, ushauri na mapendekezo yote yaliyotolewa na viongozi na kwamba wanakwenda kuyatekeleza kikamilifu ili mwaka wa fedha ujao wasiwe na hoja kabisa.
Post a Comment
0 Comments
MEDIA CLIMATE AND GENDER JUSTICE
CRDB BANK ACCOUNT-01J2058535400 ,LIPA NAMBA 54269119-VODACOM
TAFUTA HABARI HAPA
JAMBO MALTA APPLE
Kunywa Malta ya Apple kutoka Jambo
HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI
SOMA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 15,2024
September 14, 2024
MAHAKAMA KUU YA TANZANIA KANDA YA SHINYANGA KUANZA KUSIKILIZA KESI YA WACHIMBAJI WADOGO
September 15, 2024
ALIYETUHUMIWA KUMTOBOA MACHO MTALAKA WAKE AKAMATWA
September 19, 2024
SHYCOM ALUMNI MARATHON 2024 KUTIKISA SHINYANGA SEPTEMBA 21,RC MACHA AJISAJILI KUSHIRIKI MBIO HIZO
September 14, 2024
BUTONDO “FAMILY” WAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS SAMIA WAJENGA MRADI WA MAJI KWA FEDHA ZAO BINAFSI KUMTUA NDOO KICHWANI MWANAMKE
September 19, 2024
SOMA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 19,2024
September 18, 2024
WAUGUZI HOSPITALI YA RUFAA SHINYANGA WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MAADILI NA MIONGOZO YA UTUMISHI WA UMMA
September 19, 2024
MBUNGE BUTONDO ATANGAZA HABARI NJEMA KWA WANANCHI WA KISHAPU
September 13, 2024
SOMA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 16,2024
September 15, 2024
A DAY OF JOY AS THE AFRICAN DEVELOPMENT BANK CELEBRATES 60 YEARS
September 13, 2024
BLOG MARAFIKI
MALUNDE 1 BLOG
NAIBU WAZIRI PINDA AONYA MAAFISA ARDHI WANAOKIUKA MAADILI
MICHUZI BLOG
NAIBU WAZIRI PINDA AONYA MAAFISA ARDHI WANAOKIUKA MAADILI
HUHESO DIGITAL BLOG
NISHATI SAFI INAMUONDOLEA ADHA MTOTO WA KIKE - KIJAJI
MASENGWA BLOG
WAZIRI GWAJIMA : WAJASIRIAMALI WANAWAKE NA VIJANA CHANGAMKIENI FURSA ZA IMBEJU
FARAJA FM BLOG
MWENYEKITI VIWAWA TAIFA AELEZA VIPAUMBELE VYAKE
MITANDAO YETU YA KIJAMII
FACEBOOK
INSTAGRAM
MAKTABA YETU
2020
1090
2021
784
2022
1345
2023
1717
2024
1228
CHAGUA HABARI HAPA
Afya
45
AJIRA
2
habari
2972
magazeti
854
Makala
17
matukio
76
michezo
268
shinyanga
555
siasa
108
0 Comments