Header Ads Widget

MANISPAA YAFANIKISHA MSAKO WA WATOTO NA KUANZA DARASA LA AWALI


  Wanafunzi wa darasa la Awali katika shule ya msingi Mwenge iliyopo Manispaa ya Shinyanga

Na Kareny Masasy

MSAKO wa kuwapata watoto wenye umri wa miaka mitano walioanzishwa  vituo vya kulea  watoto mchana   (daycare centre)   badala ya kuanzishwa  darasa la awali limepata mafanikio manispaa ya Shinyanga nakufikia uandikishaji asilimia 100.

 Manispaa hiyo mpaka kufikia  Mwezi Marchi  2024  uandikishaji ulikuwa umefikia  asilimia 85 huku lengo la uandikishaji  likiwa asilimia 100.

Kaimu ofisa elimu Manispaa ya Shinyanga  Grace Kuzanza   anasema   uandikishaji  mpaka sasa wanafunzi wanaosoma darasa la awali  na darasa la kwanza ulienda ukiongezeka baada ya msako kufanyika.

Kuzanza anasema uandikishaji wa darasa la awali kwa mwaka jana ulifikia asilimia 105 na  mwaka huu  umefikia asilimia 100 ambapo wavulana asilimia  97 na wasichana asilimia 103.

Kuzanza anasema  kuanzia mwezi Oktoba 2023  hadi March 2024  wanafunzi walioandikishwa  ni 5059  wavulana ni 2457 na  wasichana ni  2602 wakiwemo  walemavu wasichana watatu na wavulana wanne  sawa na asilimia 85 .

 “Maoteo ya uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali  kwa mwaka 2024 ni wanafunzi  5947  wasichana 3000 na wavulana 2,947 na sasa imefikia lengo lililo kusudiwa”anasema Kuzanza.

Mwenyekiti wa vituo vya kulea watoto mchana Manispaa ya Shinyanga  Damari  Msuya anasema  kweli vituo vinasaidia  kulea watoto lakini wamiliki waangalie wa umri gani wanaohitajika kwa mujibu wa sheria wasiangalie pesa.

Baadhi ya wazazi watoto wao waliokuwa wamepelekwa kwenye vituo vya kulea watoto Amos Kulwa na Meridan Haule  wameridhia waanze darasa la awali  kwa mujibu wa sheria ya Elimu na Mafunzo.

 Haule anasema wazazi wanatakiwa kupewa elimu  kwani wengine sio makusudi ni uelewa tu hivyo msako wa kwenye vituo vya kulea watoto utasaidia kujua umri gani mtoto aanze darasa la awali.

Meneja wa shirika lisilo la kiserikali la  Investing  Children Societies  (ICS) mkoa wa Shinyanga Sabrina Majikata anasema umuhimu wa darasa la awali ni kumuandaa mtoto katika ujifunzaji wa maendeleo katika ukuaji wake  na kituo cha kulelea watoto ni kucheza kwa kadri ya umri wa mtoto kuanzia miaka miwili hadi minne.

“Mtoto anapozaliwa tu ubongo wake  unakuwa umefikia asilimia 25 katika ukuaji wake na anapofikisha umri wa miaka mitano unakuwa   kwa asilimia 92 hivyo   darasani anaendelea kujifunza  zaidi  vitu mbalimbali kupitia nyimbo na michezo”anasema  Majikata.

Majikata anasema mtoto anatakiwa kuanzishwa darasa la awali akiwa na umri wa miaka  mitano na akifikisha umri wa miaka sita aanze darasa la kwanza lakini mzazi analazimisha  huko  kwenye vituo aanze pia kufundishwa kusoma na kuandika.

“Mzazi unaposhindwa kumpeleka mtoto shule umri unaotakiwa  tayari umeanza kumnyima haki yake ya elimu ambayo anatakiwa kuipata akiwa mdogo”anasema Majikata..

Sera ya elimu ya mwaka 2014 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016  inaeleza darasa la awali kuwa Mwalimu mmoja  na wanafunzi 25 tu.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mwenge  Hemed  Hussein anasema Mwitikio wa darasa la awali kwa shule hiyo umekuwa mzuri  sababu maoteo kwa mwaka huu yalikuwa wanafunzi 130.

“Wazazi waliendelea kuleta watoto wao kutoka maeneo mbalimbali mpaka wamefika wanafunzi 300  mpaka kufunga shule” anasema Hussein.

Kwa Mujibu wa  Sheria  ya Mtoto namba 21 ya mwaka 2009 na sera ya Maendeleo ya Mtoto ya Mwaka ya Mwaka 2008  ni kuhakikisha mtoto anaandikishwa shule na kufuatilia maendeleo yao kwa kuwapatia mahitaji yote ya shule.

Katika Programu Jumuishi ya Taifa ya Maendeleo ya Awali ya Mtoto  PJT-MMMAM inaeleza Tanzania ni nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki kwenye elimu ya awali kuifanya kuwa ya lazima.

Katika sera ya elimu na mafunzo  ya mwaka  2014  na maboresho yake ya mwaka 2016 kuwa elimu bila malipo na kujumuisha elimu ya msingi   kuzita shule zote  kuwa na darasa la elimu ya awali kwa watoto wenye  umri wa miaka mitano.


 

Post a Comment

0 Comments