Header Ads Widget

UKATILI WA WATOTO UTAONDOKA KAMA NGUZO TATU ZITAWAJIBIKA

 UKATILI WA WATOTO UTAONDOKA KAMA NGUZO TATU ZITAWAJIBIKA


Na Estomine Henry na kareny Masasy-Shinyanga

ULINZI  na Usalama  wa watoto ni jukumu la familia, serikali na viongozi wa dini kwa kuwakupasa  kusimamia kwa umakini  ili  watoto waweze kuwa katika hali ya amani na ukuaji ulio timilifu.

Kwa kipindi cha takribani zaidi ya miaka mitano baada ya kuanzishwa kwa Mpango Mkakati wa Taifa wa Kutokomeza Vitendo vya Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kwa mkoa wa Shinyanga imeweza kupiga hatua kupunguza vitendo vya ukatili kwa watoto.

Ili kuendelea kuviondoa kabisa vitendo vya ukatili Wadau mkoani Shinyanga kupitia maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika inayofanyika kila mwaka mwezi June,16 wameshauri viongozi wa dini,familia,jamii na serikali kuungana kwa kusudio moja la kumkomboa mtoto.

Matukio mbalimbali ambayo yamekuwa yakiwakuta watoto na kuwaathiri kisaikolojia katika mwenendo wa makuzi yao ni   ubakaji,ulawiti,mimba na ndoa za utotoni ,ajira kwa watoto,mauaji ukosefu wa mazingira salama ya utoaji elimu ikiwemo migogoro ya familia.

 Maadhimisho Mtoto wa Afrika kwa mkoa wa Shinyanga  yamefanyika  Juni 19,2024 katika shule ya Msingi Didia wilayani Shinyanga,na kuhudhuliwa na Watoto,Wazazi,viongozi wa Serikali,na wadau mbalimbali wa Maendeleo,ambayo hufanyika kila mwaka Juni 16.

Maadhimisho hayo yaliamabatana na kauli  mbiu "Elimu jumuishi kwa watoto ,izingatie maarifa,maadili na stadi kazi.

Chombo cha habari za Shinyanga press club blog ,kilifanya  uchambuzi  juu ya ulinzi na usalama wa watoto kwa kutafuta maoni ya watu mbalimbali ili kuangazia hali ya utekelezaji wa MTAKUWWA ndani ya mkoa wa Shinyanga.

VIONGOZI WA DINI

Kauli za viongozi wa dini mkoa wa Shinyanga Nuhu Manoni kutoka Jumuiya ya Kikrito (CCT) alibainisha kuwa nyumba za ibada haziko kimya katika kukemea hali ya mifumo kandamizi ndani ya jamii inayoathiri watoto na wanawake.

Nyumba za ibada zina idara za wanawake, watoto na vijana na tunatumia majukwaa hayo kutoa elimu ya kutambua haki zao”anasema Manoni.

WADAU WA KUPINGA VITENDO VYA UKATILI

John Eddy kutoka shirika la WEADOA anasema familia ndiyo taasisi ya kwanza katika kusimamia hali ya maadili na mmomonyoko wa maadili kabla ya serikali na jumba za ibada kuelekeza maadili.

 Cecilia Msangwa kutoka shirika la YAWE  anasema  Mila ya Shikome iliyokuwa inatumiwa na wasukuma inatakiwa  kurejshwa ili kuweza kuwapa wanafamila nafasi ya kujadili hali ya maadili katika familia na  jamii.

Naona mila ya shikome inapaswa kurejea ili kuwapa wazazi nafasi ya kuwaonya na kujadili kuhus maadili kwa hali ya sasa,maana wazazi na walezi wamekuwa  wakitumia muda mwingi kwenye utafutaji  na kushidwa kujadiliana na  watoto wao kwa kuwaweka kwenye  uwazi wa vitendo visivyofa na vinavyofaa”anasema Msangwa.

John Shija kutoka kituo cha Msaada wa sheria mkoani Shinyanga (PACESHI) Sheria na kanuni za kusimamia ulinzi na usalama wa watoto zimeainishwa kwaajili ya kuonyesha adhabu na hukumu kwa watu wanaotenda ukatili dhidi ya watoto.

John Shija kutoka kituo cha Msaada wa sheria mkoani Shinyanga (PACESHI) 

 KAULI ZA WATOTO

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la watoto mkoa wa    Shinyanga Noelina Nicolaus akizungumza kwenye maadhimisho  ya siku ya Mtoto wa Afrika  amewataka wazazi kuacha  kuwafanyia ukatili watoto na kuwatimizia mahitaji yao yote wakiwemo watoto wenye ulemavu kutowabagua.

Nicolaus amewasihi wazazi pia kuendeleza vipaji  vya watoto wao ili wapate ujuzi na hata wanapofikia hatua ya utu uzima wapate kujiajiri wenyewe.

Ametoa wito kwa watoto wenzao wawe na  maadili mema na kuwasikiliza wazazi wao pia kutojiingiza kwenye makundi mabaya na kusababisha mmomonyoko wa maadili.

Naye, Helly Peter alikemea na kulaani tukio la kuawa kwa mtoto mwenye ualibino huko mkoani kagera,Asimwe Novart(2)

"Aliyeuwa haipaswi kwa kweli na tunapaswa kutoa elimu na tuendelea kutokomeza haya mambo mbaya,ukatili uliofanyika kwa mwenzetu haufai"anasema Peter.

JUHUDI ZA MKOA

Mkoa wa Shinyanga umeendelea kuchukua hatua madhubuti kwa ajili ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa kutunga Mpango kazi wa mkoa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto  na kuungana  ili kuwepo na mfano wa kuigwa.

Afisa Maendeleo ya jamii Mkoa wa Shinyanga,Rehema Edson ameitaka jamii,mashirika na viongozi wa dini na serikali kkungana kwa pamoja kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na kutekeleza mahitaji yao.

Naye, Mratibu wa Mtakuwwa, Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Aisha Omary anakiri kunufaika katika juhudi za kutomeza ukatili kwa Halmashauri hiyo.

“Sisi Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ni wanufaika wakubwa wa Muungano huu wa wadau na tumeshuhudia mabadiliko makubwa katika mapambano ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto”anasema Omary.

MFUKO WA WANAWAKE TANZANIA(WFT-T)

Mratibu wa Shirika la Mfuko wa wanawake Tanzania (WFT-T)  mkoa wa Shinyanga Gloria Mbia.
Baadhi ya mashirika ngazi ya Taifa wamefanikiwa kutoa ruzuku kwa asasi za kirai kwa ajili ya utekelezaji wa afua za kutokomeza ukatili mkoani Shinyanga.

Mratibu wa Shirika la Mfuko wa wanawake Tanzania (WFT-T)  mkoa wa Shinyanga Gloria Mbia anasema wamefanikiwa kutoa ruzuku 40  kwa awamu tano kwa asasi 12 za kirai kwa ajili ya utetezi wa haki za wanawake na watoto kwa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Matokeo makubwa ni hatua ya Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutenga bajeti kwa masuala ya ukatili kila mwaka”anasema Mbia.

OFISI YA MASHITAKA

Rose Kimaro Afisa kutoka ofisi ya mashitaka mkoa wa Shinyanga ,wakati wa kongamano la SHYEVAWC la mwaka 2023  anasema , ucheleweshaji wa kesi za ukatili mkoa wa Shinyanga umekuwa na kasi pindi ushahidi unapokuwa umekamilika na kurahisisha utoaji wa taarifa.

ili kurahisisha utoaji wa haki, ofisi yetu ina mpango mkakati  wa kutoa gharama za nauli na malazi kwa shaidi anayetoka nje ya manispaa ya Shinyanga.

WAZEE WA MILA

Vilevile viongozi wamila na desturi walilamikia kutoweka mila ya Shikome iliyoku ikitumiwa kama sehemu ya kujenga maadili mema kwa watoto.  Mwenyekiti wa machafu mkoa wa Shinyanga Njange kidola anasema” zamani kulikuwa na shikome  lakini sasa hivi wazazi na wakuwa bise na wakiridu majumbani usku muda wa kukaa na watoto haminani wakati wa jamii kujitafakari kufanya mabadiliko”

NGUVU YA TAPO

Mwakilishi kutoka TAPO la SHYEVAWC Musa Ngangala anasema  Juhudi zingine za mafanikio ni kuimarisha usalama na ulinzi wa watoto kupitia Umoja wa kikundi kazi cha asasi za kirai zipatazo 30 zinazotekeleza afua za kutokomeza ukatili mkoa wa Shinyanga

 Umoja wa kikundi kazi hicho ambapo  umetekeleza jukumu kwa kuzingatia maeneo manne ikiwa ni uratibu, uzuaji, utoaji wa huduma kwa wahanga wa ukatili na upelekaji wa habari na mawasiliano wa jamii.

Ni vyema kwenda mbali nakuungana na wenzako  ili kufikia malengo na nia yetu ni kuona haki inapatikana kwa wanawake na watoto”anasema  Ngangala.

VYOMBO VYA HABARI

Mwandishi wa habari  mkoani Shinyanga Kareny Masasy anaeleza mchango wa vyombo vya habari ulivyoweza kuibua na kuleta mafanikio kwa kuripotiwa matukio mengi.

 Kwa mujibu wa taarifa kutoka wizara ya afya  umeonyesha mkoa wa Shinyanga  umekuwa nafasi ya pili katika kuripoti  masuala ya ukatili wa kijinsia  na watoto ikiwa  matukio 12,300 yaliripotiwa.

Waandishi tumepaza sauti zetu kwenye vyombo vya habari kupitia mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto kufikia mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla”anasema Masasy

JESHI LA POLISI

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga Janeth Magomi,akizungumza wakati wa kampeni ya ONGEA NAO ,aliwahi kusema,matendo ya ukatili wa kijinsia ni pamoja na ubakaji, ulawiti vipigo, kutelekeza familia, kutumikisha watoto na kuwazorotesha masomo, lugha za matusi na ndoa za utotoni huku akiyataja madhara ya ukatili wa kijinsia kuwa ni pamoja na vifo, mimba za utotoni, maradhi yanayosababishwa na ngono mfano UKIMWI, ulemavu wa kudumu, kuongezeka kwa watoto wa mitaani, umaskini, msongo wa mawazo, na migogoro ya kifamilia.

"Jeshi la Polisi tunawataka wanafunzi, wananchi ,wadau kutambua kuwa mnawajibu wa kupaza sauti na kutoa taarifa za uhalifu katika vyombo vya sheria ili kukomesha vitendo hivyo katika jamii inayozunguuka, kwani jukumu la ulinzi na usalama ni la kila mwananchi",amesema Kamanda Magomi

"Pia mnapaswa kutambua mifumo mbalimbali ya utoaji taarifa za ukatili wa kijinsi ambayo ipo katika jamii zetu. Mifumo hiyo ni pamoja na viongozi wa dini, dawati la jinsia polisi, ustawi wa jamii, viongozi wa serikali za mitaa au mtu yeyote anaaminika anaweza kutoa msaada. Hivyo basi niwaombe au nitoe rai kwa wananchi wote wa mkoa wa Shinyanga tuungane kwa pamoja mkoa wetu uendelee kuwa salama" Amesema Magomi

CHAMA CHA MAPINDUZI

Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Shinyanga Rehema Namanilo amesema takwimu za kufanyiwa ukatili zinatisha ni vizuri jeshi la polisi likatenda haki likasimamia ipasavyo angalau likawabana wahalifu wakapewa adhabu yao na litoe elimu kuanzia ngazi ya vitongoji ili watu hao waliokandokando ya mji wawe na uelewa wa kutoa ushahidi.

MWISHO.

MATUKIO MBALIMBALI YAKIENDELEA WADAU WA KUTOKOMEZA UKATILI










 MICHEZO MBALIMBALI YA WATOTO IKIENDEELA WAKATI WA MAADHIMIOSHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA-MKOA WA SHINYANGA 


Post a Comment

0 Comments