Header Ads Widget

MIPANGO YA SERIKALI,WADAU WAPUNGUZA VIFO VYA WATOTO WACHANGA KAHAMA

 Watalaamu kutoka vitendo  tofauti  sekta ya Afya  wakiwa katika mdahalo wakielezea namna walivyopunguza vifo vya watoto wachanga mkoani Shinyanga.

Na Kareny  Masasy,

SABABU  ya vifo kupungua Manispaa ya Kahama  mkoani Shinyanga  nikutokana na  serikali kuwa na mipango madhubuti pamoja na  kuungana na wadau mbalimbali  wanaotekeleza kupunguza vifo  vya watoto wachanga  na wajawazito.

Sera ya afya ya mwaka 2007 imewekeza katika kuboresha  uhai wa mtoto kupitia utoaji wa huduma za afya bure kwa kina mama wajawazito  na watoto chini ya miaka mitano.

Uwekezaji wa serikali katika uhai wa mtoto unaonekana dhahiri kwenye kupungua kwa vifo vya watoto kati ya mwaka 2010 hadi 2015 ambapo kiwango cha vifo vya watoto wachanga  kuanzia siku 0 hadi 28 vimepungua  kutoka vifo 40 hadi vifo 25 kwa kila kizazi hai 1000.

Mratibu wa afya ya Mama na Mtoto mkoani Shinyanga Halima Hamis anasema kumekuwepo na vituo vya kutolea huduma ukijumlisha na hospitali za Halmashauri na Rufaa  243 na vyote vinahuduma ya mama na mtoto bure.

Pia mkoa huu  kuna vituo 35 vya kutolea huduma  ambapo vituo vya afya pekee viko 25 na Hospitali ni 10  ambapo  mahudhurio ya kliniki  kwa mjamzito  wiki  ya 12 za mwanzo    yamefikia asilimia 34 ukilinganisha na kitaifa asilimia 60  yapo mafanikio.

Hamis anasema kuongezeka kwa  vituo vinavyotoa huduma ya dharura ya upasuaji  kwa wajawazito  katika kila kata  kwa mujibu wa sera ya afya   ya mwaka 2007 inavyoeleza.

“Ipo huduma ya M-Mama ambayo  ilikuwa ikifadhiliwa na Mdau na sasa Halmashauri   ndizo zimechukua jukumu hilo baada ya Mdau kuisha mkataba wake”anasema Hamis.

“Halmashauri hizo zimekuwa zikitenga fedha kwaajili ya  kusafirisha  wajawazito na watoto wenye changamoto kwa  utaratibu wa kushirikiana na viongozi wa mtaa,vitongoji,vijiji  ambapo wao  ndiyo wanatafuta gari na dereva wanao waamini na malipo yanalipwa kutoka Halmashauri”anasema  Hamis .  

Halima anasema mpango wa M-Mama ulianza katika halmashauri wilaya ya Shinyanga kama majaribio  kwa mwaka mmoja ikaonekana kufanya vizuri na sasa mpango huo upo kwenye halmashauri  zote sita za mkoa.

Halima anasema njia ya uzazi wa mpango  inazuia vifo kwa asilimia 40 ambapo kila Zahanati au kituo cha afya kuna huduma hiyo wanapokwenda kliniki wanapewa elimu.

Wadau wanaotekeleza uzazi wa mpango kwa mkoa wa Shinyanga  ni Mariestopes na Pathifinder  wamekuwa wakishirikisha  baba na mama katika utoaji elimu

Pia kuna Mradi wa kitita salama  una mdau wake  na Thamini uzazi  Salama nao mdau wake  wenye malengo ya kupunguza vifo vya watoto wachanga.

Daktari bingwa wa magonjwa ya watoto kutoka hospitali ya Rufaa ya Mkoa  Justina Tizeba anasema  asilimia 10 ya watoto wanaozaliwa  wanahitaji kusaidiwa zaidi wengine wanazaliwa njiti.

Dk Tizeba anasema sababu ya vifo vya watoto wachanga vinazuilika  kina baba nao washirikiane na mama  katika  huduma ya mtoto pindi  bado mchanga.

Daktari bingwa wa Magonjwa ya wanawake  kutoka hospitali ya rufaa ya Mkoa   Dk Agustino Maufi anasema  asilimia 57 ya wanawake wanaobeba mimba wanakuwa na viashiria vya upungufu wa damu.

Dk Maufi anasema mpango uliokuja  umeongeza mahudhurio ya kliniki kwa wajawazito badala ya mahudhurio manne yamekuwa nane nakuhakikisha kila hudhurio  anapimwa wingi wa damu.

“Mjamzito  huyo ataweka  mahusiano mazuri na watoa huduma na atakapo hudhuria kliniki  mara zote hawatapata changamoto  nakuendelea kuokoa vifo vya watoto wachanga”anasema Dk Maufi.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Annamringi Macha anasema   kwa kipindi cha miaka mitatu serikali imeleta  zaidi ya Shilingi Bilioni 30 kwenye sekta ya afya  na kumekuwepo ongezeko la vituo vya afya 37 Zahanati  50 nakufikia vituo vya kutoa huduma ndani ya mkoa 270.

Waziri  Afya Ummy Mwalimu  anaeleza  kuwa ongezeko hilo la matumizi ya huduma za kliniki wakati wa ujauzito limetokana na kubadilika kwa mwongozo wa huduma muhimu wakati wa ujauzito kutoka mahudhurio ya kila baada ya miezi mitatu na kuwa mahudhurio ya kila mwezi.

Pia kuna  Kuongezeka la   wahamasishaji  ambao ni wahudumu ngazi ya jamii  kuanzia ngazi za vitongoji  juu  ya uhumimu wa wajawazito kuhudhuria kliniki .

“Takwimu zinaonesha kuwa kati ya wajawazito 1,784,809 ni wajawazito 656,040 sawa na asilimia 37.6 walianza kupata huduma za wajawazito chini ya wiki 12 za mwanzo wa ujauzito ikilinganishwa na asilimia 36 ya kipindi kama hiki mwaka 2020,” ameongeza.

Malesela anasema  Manispaa ya Kahama  Vituo sita  vimepata  wahudumu   waliopitia mafunzo na kupitia mradi  wa Kitita cha Uzazi Salama  (SBBC)  wadau hao wameajiri watu wanaofuatilia   takwimu  za  mama wanaojifungua  salama pamoja na watoto  na waliopoteza maisha pia .

“Takribani   kwa siku watoto wanazaliwa  kwa hospitali ya manispaa ya Kahama ni  35 hadi 40  na  kwa mwezi watoto zaidi ya 1000 na kila mtoto anaweza kuzaliwa na changamoto zake”anasema Malesela.

Watoto wengi wametambulika na kupona  ndiyo maana tulikuwa tunaendelea kuona vifo vya watoto wachanga vinazidi ikiwa mwaka 2020 kulikuwa na vifo  382 vya watoto wachanga.

Zubeda Galula  mkazi wa Manispaa ya Kahama Kata ya Majengo anasema alipata changamoto ya uzazi wakati anajifungua akapata rufaa ya kusafirishwa  kuletwa Shinyanga mjini amefurahi kuokolewa yeye na mtoto wake.

Mariamu Joshua ambaye ni wifi yake  Zubeda anasema  alielezwa awali kabla ya kujifungua njia haifunguki  lakini waliona wauguzi hali inazidi kuwa mbaya walimsafirisha na sasa anaendelea vizuri na mtoto.


Post a Comment

0 Comments