Header Ads Widget

TAKUKURU SHINYANGA KUTHIBITIIVITENDO VYA RUSHWA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA, WABUNGE,MADIWANI NA MAWAKALA WABAINISHWA KATIKA RIPOTI.

 

TAKUKURU SHINYANGA KUTHIBITI VITENDO VYA RUSHWA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA, WABUNGE, MADIWANI NA MAWAKALA WABAINISHWA KATIKA RIPOTI.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Shinyanga  Donasian  Kessy

Na mwandishi  Wetu,

TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru)  mkoa wa Shinyanga imejipanga kuthibiti vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwaka huu (2024)  kwa kutoa  elimu kwa wadau juu ya madhara ya rushwa.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Shinyanga. BW. Damian Kessy ameeleza hayo julai 31, 2024 katika mkutano wake na vyombo vya habari wakati akiwasilisha taarifa yake kwa kipindi cha miezi mitatu yakuanzia April hadi Juni.

Takukuru itatoa elimu kwa wadau mbalimbali ikiwa ni wajumbe ambao ni wapiga kura, Wagombea,wasimamizi wa uchaguzi, viongozi wa dini , waandishi wa habari na kutoa elimu kwa wananchi wa kata zote 130 za mkoa wa shinyanga ili kuhakisha tunawajengea uelewa wa kubaini vitendo vya rushwa kabla na wakati wa uchaguzi “anaeleza  Kessy

Anaongeza pia “Takukuru kuchukua hatua za kisheria pale itakapobainika Wagombea au wapambe wanajihusisha na vitendo vya rushwa”

Hata hivyo Mwandishi wa Makala hii anaeleza uchaguzi wa serikali za mitaa umekuwa na hali ya matukio ya mianya ya rushwa kwa kila nyakati na hali inayofanya kudumaza kwa ukuaji wa demokrasia nchini  na kutopatikana viongozi bora.

Mwandishi huyo anaeleza, Matokeo ya utafiti ya Takukuru juu ya mianya ya rushwa katika uchaguzi wa mwaka 2014 yalibainisha viashiria vya rushwa.

Kwa mujibu  wa taarifa ya mianya ya rushwa serikali za mitaa kupitia  tovuti ya Takukuru inaonyesha  kwa  mwaka 2014, Wananchi walidai  walishuhudia vitendo vya rushwa katika kampeni za uchaguzi wa serikali za Mitaa 2014 ambapo, asilimia 54.2 walieleza kuwa hakukuwa na vitendo vya rushwa na asilimia 42.9 walieleza kuwepo kwa vitendo vya rushwa.

 Tovuti hiyo ilionyesha  asilimia 32.9 ya wahojiwa walieleza  kulikuwa na vitendo vya rushwa vilivyohusiana na ugawaji wa fedha taslimu, asilimia 9.8 walieleza kuwepo kwa ugawaji wa kanga na Tshirt na asilimia 26.8 walieleza kuwa wapiga kura walipewa vinywaji na vyakula.

Kwa mujibu wa tovuti  hiyo inaeleza utafiti wa mwaka 2014, ulibanisha vitendo vya rushwa katika mchakato wa kampeni za serikali za mitaa na vitendo hivyo  vilivyohusisha ugawaji wa mifuko ya saruji, ugawaji wa mipira ya miguu, harambee kanisani, kutoa pikipiki na michango katika misiba.

Pia baadhi ya maeneo vitendo vya rushwa vilijidhihirisha kwa ugawaji wa chumvi na vitu vingine vya thamani siku ya kupiga kura.

Pia ugawaji vitu vya rushwa kulifanyika kwa kupelekwa majumbani kwa wapiga kura au wakati wapiga kura wanaelekea vituoni kupiga kura na  katika matukio hayo, utafiti ulibaini  shughuli hizo ziligharamiwa na baadhi ya wagombea na katika baadhi ya maeneo, mawakala wa wagombea walitumika.

Mwaka huo wa uchaguzi ulionyesha  baadhi ya maeneo madiwani na wabunge walishirikiana na baadhi ya wagombea kuwahonga wapiga kura, Madiwani na wabunge  walishirikiana na  wagombea kwa matarajio kuwa watakaposhinda watawasaidia katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

MWISHO.


Post a Comment

0 Comments