Header Ads Widget

TAPO LA SHYEVAWC LIMEPITISHA MPANGO KAZI WA SHUGHULI ZA UTETEZI WA HAKI ZA WANAWAKE NA WATOTO KWA JULAI –DESEMBA 2024.

 

TAPO LA SHYEVAWC LIMEPITISHA MPANGO KAZI WA SHUGHULI ZA UTETEZI WA HAKI ZA WANAWAKE NA WATOTO KWA JULAI –DESEMBA 2024.

Na mwandishi wetu.

Kikundi cha asasi za kiraia mkoa wa Shinyanga  kinachotambulika kwa jina la SHY EVAWC) kinachoshughulika na kutokomeza ukatili mkoa wa Shinyanga kimepitisha mpango kazi  wake kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake kwa kipindi cha julai hadi desemba 2024. Kikundi hicho kinaundwa na asasi zipatazo 30 zinazotekeleza afua za MTAKUWWA kimekuwa ni msaada kwa jamii na serikali dhidi ya vitendo vya ukatili mkoa wa Shinyanga.

Mwenyekiti wa TAPO la SHYEVAWC,Jonathan Kifunda  alisema  ni wajibu kwa kila asasi kuendelea na majukumu yake ya kutetea haki za wanawake na watoto kwa kuzingatia Mpango kazi wa Taifa wa Kutomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na watoto(MTAKUWWA), Hayo yalibainishwa katika kikao cha robo mwaka cha kikundi kazi hicho kilichiofanyika manispaa ya Shinyanga julai 2,2024.

“Mpango kazi wa MTAKUWWA ni mpana sana na kila mwanachama analo jukumu la kuendelea kutekeleza shughuli zake kwa kuchomoa kile anachoweza katika mpango huo wa Taifa ili kusaidia serikali na jamii dhidi ya masuala ya ukatili kwa mkoa wetu

Mwenyekiti wa SHYEVAWC, Jonathan Kifunda akizungumza katika kikao cha robo mwaka cha TAPO.

TAPO hilo limepitisha mpango kazi wake unajikita kutetea haki za wanawake na watoto kupitia timu iliyogawanyika katika mihimili minne ikiwa ni uratibu(coordination),kuzuia(prevention), kutoa huduma kwa wahanga(response) na mawasiliano kwa jamii(communications). Ambapo kila muhimili ulipata nafasi ya kuwasilisha mpango kazi wake na kupatiwa baraka za wajumbe.

Wajumbe wa TAPO hilo walionesha nia ya dhati ya kuwa na mikakati imara ya kuimarisha uendelevu wa TAPO hili kwa kutoa maoni ili kufikia malengo waliyojipangia kwa ustawi wa maendeleo ya utetezi wa  haki za wanawake na watoto.

Mjumbe wa TAPO hili, John Shija alishauri chanzo za msingi wa kuwepo kikundi kazi hicho ni kuendelea kutoa nafasi za watu walio na hiari zaidi na kujifunza zaidi kwa wengine waliokwama ni vitu gani waliviweka na kuwafanya kukwama.

“Tulianza kwa takafari kubwa juu ya TAPO hili kwa kutazama historia ya kufa kwa matapo mengine na kuwa waangalifu katika kuepuka mambo yanayoweza kuwa ni kikwazo na hadi leo tuko hapa,ni vema tukumbuke ile nia ya awali ili tuendele kuimarika “anasema Shija.

John Shija-kutoka shirika la PACESH akizungumza.

Naye Catherine Kalinga kutoka kitengo cha utoaji huduma kwa wahanga anashauri kuwepo na mfumo wa kidigitali wa ufatilia wa kesi zote za ukatili kwa TAPO hili ili kuwa na kumbukumbu za matukio.

Nishauri tuwe na mfumo rafiki wa pamoja utakaosaidia kutambua mwanzo hadi mwisho wa kesi za ukatili ili tuwe na njia rahisi ya kufatilia”anasema Kalinga

Kwa upande wake Peter Amani kutoka Shirika la COED –Tanzania ameshauri ushirikiano zaidi na vyombo vya habari baina ya kitengo cha mawasiliano na habari ili kupaza sauti zaidi kwa utetezi wa haki za wanawake na watoto.

“Ni vema tuendele kuimarisha mawasiliano kwa umma ili wajue shughuli zetu kwa upana na tuwape mahitaji yao kwa wao kutambua akaunti zetu za mawasiliano za SHYEVAWC na pia kuongeza wigo wa mashirikiano na vyombo  ya habari.

Peter Amani kutoka Shirika la COED-Tanzania akichangia mada.

Vile vile, Mratibu wa Mfuko wa wanawake Tanzania-mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia,  anasema mabadiliko ya wafadhili ni kuhitaji uwepo wa umoja kama  huu na wanafatilia maendeleo yetu, Wanachama wote watumie dhamana ya Tapo hilo kutafuta fursa ili kutetea haki za wanawake na watoto na pia waendele kujengea uwezo katika maeneo mbalimbali.

Mratibu wa Mfuko wa wanawake Tanzania-mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia, 

Pia TAPO hilo liliweza kupokea wanachama wapya kwa ajili ya kujiunga kwa majukumu ya utetezi wa haki za wanawake na watoto. Ambapo wanachama wapya Nacopha konga manispaa ya Shinyanga, AGDC, na Lifeline walipokelewa.

Katibu wa NACOPHA KONGA, Manispaa ya Shinyanga Edson Justine, Amesema ni muda muafaka wa kutokomeza ukatili na unyanyasaji wa watu wanaishi na virusi vya ukimwi kwa kujiunga na Tapo hilo.

Katibu wa NACOPHA KONGA, Manispaa ya Shinyanga Edson Justine,

Mkurugenzi wa shirika la Life line,Dk. Kulwa Meshaki anasema,amekuwa na jitihada na kusumbua uongozi ili ajiunge kwa kuona na kuridhika na makubwa yanayo fanya na kikundi kazi hicho.


Mkurugenzi wa shirika la Life line,Dk. Kulwa Meshack akichangia mada

Mwamabadiliko kata ya pandagchiza, Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Shadrack Ngome anasema yuko tayari kushirikia na SHYEVAWC ili kutoa elimu kwa jamii kupitia vikundi na mikutano ya hadhara.

Mwanamabdiliko ,Shadrack Ngome  kutoka kata ya pandagchiza akijitambulisha kwa wajumbe.

MATUKIO KATIKA PICHA.

Katibu wa SHYEVAWC-Veronica Massawe akitoa maelekezo ya kikao cha robo mwaka cha SHYEVAWC

Vicent Laurent,Mwenyekiti wa uzuaji matukio ya ukatili akiwasilisha mpango kazi

Mwakilishi wa muhimili wa utoaji huduma (response) Catherine Kalinga, akiwasilisha mpango kazi 

Mwakilishi wa timu ya uratibu,(coordination),Glory Mbia akiwasilisha mpango kazi.

Mwenyekiti wa muhimili wa mawasiliano na habari,(communications),Estomine Henry  akiwasilisha mpango kazi


TIMU ZA VIKUNDI-KUJADILI MPANGO KAZI-

Muhimili wa uratibu (coordination) ukijadili mpango kazi.
muhimili ya kuzuia(prevention) ukijadili mpango kazi 
Muhimili ya utoaji huduma (response)ukijadili mpango kazi.

WAJUMBE WAKICHANGIA MADA HAPA CHINI.


WAJUMBE WAKIFATILIA KIKAO-SHYEVAWC









WANAMBADILIKO KUTOKA NGAZI YA JAMII WAKITOA SALAM ZAO





Post a Comment

0 Comments