Header Ads Widget

JAMBO WAZINDUA SURA MPYA YA BIDHAA ZAKE


JAMBO WAZINDUA SURA MPYA YA BIDHAA ZAKE

Na Marco Maduhu,SHINYANGA
KAMPUNI ya Jambo Group imezindua sura mpya ya bidhaa zake, kuwa na muonekano mpya zaidi wa kuvutia kwa wateja wake.

Hafla ya uzinduzi huo umefanyika jana kwenye kiwanda hicho ukiongozwa na Mkurugenzi Nassoro Salum Hamis pamoja na Meneja Mkuu wa Jambo Fm ambaye pia ni msimamizi wa chapa group Nickson Geogre, huku ukihudhuriwa na wananchi pamoja na wafanyakazi wa jambo.
Geogre akizungumza wakati wa uzinduzi huo, amesema kampuni ya jambo group imetimiza miaka 20 sasa, hivyo wameona ni vyema kuwa na muonekano mpya wa bidhaa za jambo,ambazo zitawavutia wateja wake, na kwamba ukitumia bidhaa za jambo ni kupata furaha yenye maisha mazuri.

“muonekano huu mpya wa bidhaa zetu ni jambo ilele, hivyo wateja wetu wakiona mabadiliko wasizani siyo sisi,na tuna msemo wetu unasema “ jambo hawa ni sisi”
Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo, wamepongeza muonekano mpya wa bidhaa za jambo, huku wakitoa wito kwa watanzania kwamba wawaunge wawekezaji wazawa kwa kununua bidhaa zao.

Kauli mbiu ya uzinduzi wa sura mpya bidhaa za jambo inasema “Jambo hawa ni sisi,dukani mpaka nyumbani,sisi ndio sura mpya ya furaha na maisha mazuri”

Post a Comment

0 Comments