Header Ads Widget

MWANAFUNZI ADAIWA KUBAKWA NA JIRANI KISIMANI




Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 13, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Chibe, imedaiwa kubakwa na Juma Mussa Mmhela anayekadiriwa kuwa na umri wa Miaka 45, mkazi wa kijiji cha Chibe Manispaa ya Shinyanga.













Aidha, ameiomba serikali ichukue hatua kali za kisheria dhidi ya mtuhumiwa ili iwe fundisho kwa wengine.

Mwenyekiti wa mtaa wa Chibe, Bwana Kashinje Misana, amethibitisha kupokea taarifa za tukio hilo na kulaani vikali kitendo hicho akisema, "Hili ni tukio la kikatili na lisilovumilika watoto wetu wanapaswa kulindwa na jamii, siyo kudhulumiwa."

viongozi wa jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA), wakiwemo katibu wa SMAUJATA Kanda ya Ziwa Bwana Daniel Kapaya, mwenyekiti wa SMAUJATA Manispaa ya Shinyanga Mwarabu Mwimbili, na katibu wa SMAUJATA Manispaa ya Shinyanga Bi. Husna Maige.

Viongozi hao wa wamelani vikali tukio hilo huku wakihimiza wananchi kushirikiana na vyombo vya sheria katika kutoa taarifa za matukio ya ukatili.




Viongozi wa jumuiya ya SMAUJATA wakiwa na Mariam Maganga Masabo shangazi wa mtoto huyo, ambaye ni mjumbe wa serikali ya mtaa wa Chibe na pia katibu wa Umoja wa Wazazi (UWT) kata ya Chibe. 


Post a Comment

0 Comments