Header Ads Widget

TAKUKURU MKOANI SHINYANGA YAWATAKA VIONGOZI WA DINI KUWASHAURI WAUMINI KUJIANDIKISHA NA KUPIGA KURA

 

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoani Shinyanga imewataka viongozi wa dini kuwahamasisha waamini wao kujiandikisha na kupiga kura sambamba na kuchukua tahadhari juu ya vitendo vya rushwa vinavyoweza kujitokeza katika mchakato mzima wa maandalizi ya uchaguzi huo huku baadhi ya wazee maarufu wa Mkoa uo wakidai kuwa zoezi la kujiandikisha linaenda kwa kusuasua hali ambayo inaweza kuathiri uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 mwezi wa 11 mwaka huu.

Na Mwandishi wetu kutoka Nkoani Shinyanga.

Hata hivyo Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa shinyanga  Bw. Donasian Kessy ametoa wito kwa viongozi wa Dini ambao wamehudhuria semina iliyoandaliwa na TAKUKURU na kufanyika katika ukumbi wa taasisi hiyo kuisaidia serikali kuwaomba waumini wao kushiriki mchakato mzima wa zoezi la uchaguzi kwakua wao ndio wenye dhamana ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Alley juma ni mwenyekiti wa Baraza la Bakwata mkoa wa shinyanga amesema utaratibu uliowekwa na serikali kuweka vituo vya kujiandikishia tofauti na utaratibu wa zamani wa maofisa waandikishaji kupita nyumba kwa nyumba umekuwa changamoto inayosababisha watu kutojitokeza kujiandikisha huku mwenyekiti wa Makanisa ya CCT mkoa wa shinyanga Mchungaji Nalinga Najulwa akiitaka serikali kutumia siku zilizobaki kutangaza mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba kuwahamasisha wananchi kujiandikisha ili kuepuka changamoto zinazoweza kukwamisha uchaguzi huo.

Mchungaji Yohana Ernest Nzelu ni Askofu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria ametoa wito kwa waumini wa Kanisa la KKT Pamoja na wananchi wote kutopuuzia zoezi la kujiandikisha na kupiga kura kwakuwa ndiyo fursa pekee ya kuchangua viongozi watakaosaidiana na Serikali kusimamia miradi ya maendeleo kwa ajili ya maendeleo ya jamii yote ya Taifa la Tanzania.

Hata hivyo Pamoja na jukumu la TAKUKURU la kuzuia na kupambana na rushwa imeshauria kuchunguza kwa undani zaidi mambo yanayofanywa na viongozi baadahi wenye nafasi kubwa serikalini yanayoashiria rushwa kwakuwa yanaweza kuutia dosari uchaguzi huo.


Pamoja na hayo viongizi wa Dini wameitaka Serikali kujenga ofisi za TAKUKURU kwenye ngazi za chini vijijini ngazi ya kata na vijiji kwakuwa huko pia vitendo vya Rushwa vinafanyika hususani rushwa ya Ngono.

Hata hivyo Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU imewakumbusha Wananchi kauli mbiu ya Taasisi hiyo inayosema kuwa “Jukumu la kupambana na rushwa ni lako na langu,sote kwa Pamoja tushiriki kupambana nayo na kuitokomeza





Viongozi wa dini wilaya ya Shinyanga wakifatilia mada za rushwa katika uchaguzi.



Watendaji wa Takukuru wakiwakilisha mada za kuhusu hali ya rushwa katika uchanguzi.

Post a Comment

0 Comments