![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgex-QJmvLK15gvpbSW8juDVGYI8Mkkfk_34LLU02MLrPvJoOqFquphVsFa_6Ix6wc2AygL0FTnDndx8YVa715F4WGRNLr9Dx3siJyE0Q6-SmxfSslt4suuXAYHO0edYCOB5NOL3DOcEpMmjp9MyJsDAGc4rKGpFh6-o_3NkCTbnxvozK_3sW5m_FKwpEQ/s600/BARAZ4A.jpg)
Hayo yamebainishwa leo Februari 7,2025 kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani cha Robo ya Pili, wakati wa uwasilishwaji wa Taarifa ya Kamati ya Mipango Miji na Mazingira.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8nJjq2U2woAtTbs45ojroXKvIKhv3a6i7YFfSh4xD7tOsHc-dr3Wc7-02duq7YG4YqEZUhZOToe3j6HUFX8yYHEWX1Pq8EUOg7lkFS6RELfKrh0Zsgp8TFuSGwKoOlMI2p0lr8lvrYV4da8VX-kRsFMB4hs0DlVELwavVii9LasoMdVWeZva9uCWQIR0/s600/MADIWANI%208.jpg)
Amesema ili kuendelea kulinda hadhi ya Manispaa hiyo kuwa mji msafi na kulinda tuzo ya usafi wa mazingira kutoka wizara ya afya, kwamba wameweka mikakati madhubuti ya kuendelea kuimarisha hali ya usafi zaidi, pamoja na kukumbusha wananchi kufanya usafi katika maeneo yao.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcii9SXE6haoVFU5QzgQZsvcDOwa72RXMgfg5O4kVuzvZLLNCNiFajqx0wuMfbhATqFWvNaJl-GdNroy6nc_VEsewW2994-I7meiGsJgKlg8lvOgidEgBaRpnqYhXHyvKBsnNByMeCDkmjZVD3sh-UaOzx1ugiU44qtmz6juMVOA2PooKT9P4oJ1qOOrs/s600/MEYA2.jpg)
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko, naye amesisitiza suala la usafi kwenye mji huo, na kwamba uchafu kwa sasa umeanza kuonekana, ili kuendelea kulinda heshima yao ya kupata tuzo ya ushindi wa usafi wa mazingira ngazi ya miji.
Awali Diwani wa Kizumbi Rubeni Kitinya, aliuliza swali juu ya mikakati ambayo manispaa ya Shinyanga imechukua, dhidi ya kuimarisha hali ya usafi wa mazingira, ambapo kwa sasa hali imeanza kuwa siyo nzuri kutokana na maeneo mengi kuwa machafu.
Amewalalamikia pia Mawakala wa kukusanya uchafu,kuwa wameshindwa kufanya kazi zao vizuri, huku wakati wa uzoaji wa Taka kwenye Magari yao kupeleka dampo, kwamba wamekuwa wakiagusha uchafu hovyo barabarani na kusababisha mji kuonekana kuwa mchafu.
TAZAMA PICHA👇👇
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akizungumza kwenye kikao cha Baraza.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi4lhwH7BvVbk25el23G0iX4CfziuZPOHaCMKo0Yxe3xBUE70WAZ3LnPLc-I3SbYdT0YM9DQRVKSzLfKgBGfTgoEqTlOn_wefWYDx7yT5YtxlG5uEYkpVtxyDGxg-zWEpSGQqp5lSSioY0_PezKD-LMEp1KHXpFookZI5Gyqxee4OwV10vFbtM5KjIndr8/s600/KAIMU%20MD.jpg)
Kikao cha Baraza la Madiwani kikiendelea.
Diwani wa Kizumbi Rubeni Kitinya akiuliza swali kwenye kikao cha Baraza la Madiwani.
Baraza la Madiwani likiendelea.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464