MASENGWA YAENDELEZA KAMPENI YA UTUNZAJI MAZINGIRA KWA UPANDAJI MITI


Na Mwandishi wetu.

AFISA   Elimu  wa kata ya Masengwa   Halmashauri ya  Wilaya  ya Shinyanga  Shabani Nzila  ameongoza  zoezi  la upandaji  wa miti katika shule tano  za msingi na Sekondari.

Zoezi hilo liliendeshwa tarehe  18/02/2025   na Afisa huyo   katika mida tofauti tofauti baada ya kutoa miti  na kuhamasisha wanafunzi wa  shule hizo kushirikiana na walimu katika kuipanda.

Afisa Elimu Mwalimu  Nzila  amezitaja shule hizo  kuwa ni Bubale,Ikonda, Masengwa shule ya msingi na Sekondari ,Ilobashi .

“Walimu  ambao hawakuwa na vipindi  kwa siku hiyo na  wanafunzi tumeshirikiana vizuri   tumeweza kupanda   na kila mtu alikuwa akipanda miti miwili”amesema Mwalimu  Nzila.

  Mwalimu Nzila  amesema  wamepanda miti  hiyo pia  katika ofisi ya mtendaji wa kata  kuhakikisha mazingira yanakuwa mazuri.



Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464