LISSU AELEZA MAUMIVU WALIOSHINDWA UCHAGUZI CHADEMA


Lissu aeleza maumivu ya walioshindwa uchaguzi CHADEMA


Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu akizungumza na waandishi wa habari wa Nipashe nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu ameeleza kutambua maumivu ya walioshindwa uchaguzi ndani ya chama hicho na kutaja mikakati ya kutibu majeraha yaliyotokana na uchaguzi huo.

Akizungumza na waandishi wa Nipashe waliofika nyumbani kwake Jumapili iliyopita, Lissu alisema ameliachia Baraza la Wazee la Chama hicho (BAZECHA) kazi ya kuponya majeraha hayo ili kurejesha umoja ndani ya chama hicho.

“Tuna baraza la wazee ambao nimewapa jukumu la kusaidia kuponya majeraha, majeraha ya uchaguzi kama yalivyo majeraha mengine hayaponi siku moja” alisema Lissu.


SOMA HAPA ZAIDI CHANZO NIPASHE
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464