Neema Sawaka,Kahama
CHAMA cha Walimu Wilaya ya Ushetu Mkoani Shinyanga kimefanya uchaguzi nakumchagua Juma Nyakanyenge kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa mara nyingine baada ya kumshinda mpinzani wake Petro Basili.
Katibu wa CWT Mkoa
wa Shinyanga Kizito Shuli
ametangaza matokeo hayo leo tarehe 24/03/2025 baada
ya kufanya uchaguzi katika Mkutano Mkuu wa uchaguzi nakuhudhuliwa na wajumbe zaidi ya 140
ambapo Nyakanyenge alipata kura
78 huku mpinzani wake akipata kura 68 na kura moja iliharibika.
Shuli
aliendelea kutangaza matokeo ya nafasi
ya Mwekahazina alishinda
Wambura Yudas aliyerudia nafasi
hiyo kwa mara nyingine huku akiwashinda
wapinzani wake wawili ambao ni Ally Nurali
na Frank Zoto
Pia ameendelea kutaja Kundi la uwakilishi
walimu vijana aliyeshinda ni Mwalimu Johanes Samweli na kundi la uwakilishi walimu wanawake
aliyeshinda ni Mwalimu Ana Nzingu.
Mwalimu Said
Soja alipata nafasi ya uwakilishi wa walimu wenye ulemavu kwa kupigiwa kura za ndiyo na hapana
ambapo alipata kura 139 za ndiyo huku kura tano zikizema hapana ambapo kinyang’anyiro hicho alikuwa
hana mpinzani .
Baada ya
kutangaza matokeo hayo Katibu Shuli amesema matokeo yaliyopatikana wayakubali nakuvunja makundi
waliyokuwa nayo nakutakiwa kuwa wamoja.
Mwenyekiti Nyakanyenge wakati akitoa shukrani kwa wajumbe amesema sasa kazi imeanza
ataendelea kutoa ushirikiano aliokuwa nao zamani kuhakikisha haki na maslahi ya walimu
vinaendelea kuwepo.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464