Na Kareny Masasy, Msalala
WANAWAKE wengi wamekuwa hawafuati utaratibu wa kiafya
ikiwemo lishe bora huku wakitarajia kubeba ujauzito na kutegemea kupata mtoto mwenye akili hilo
litakuwa suala gumu.
Hayo
yamesemwa tarehe 5, March,2025 na Afisa elimu Afya kutoka halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani
Shinyanga Peter Ngazo kwenye kongamano la wanawake lililofanyika kata ya Bugarama.
Ngazo amesema wazazi wengi wamekuwa wakidai mimba walizobeba niza bahati mbaya matokeo yake wanapoanza kuzilea mimba hizo
huku mtoto akiendelea kukua tumboni
anaendelea mama naye anakuwa akila udongo wa pemba.
“Mtu
anayekuwa udongo wa pemba huyo anaupungufu wa madini ya zinc ambayo yanapatikana kwenye mboga za majani
ambapo mboga hizo za majani kama mchicha
watu wamekuwa wakidharau nakuona kama hauna faida mwilini angalau
angekuwa nyama”anasema Ngazo.
Ngazo amesema utafiti umeonyesha wanawake wenye umri wa kuzaa wamekuwa wakibeba mimba kabla ya kujiandaa ndiyo maana matatizo yamekuwa yakitoke kwa kupatwa na hali ya upunguvu wa madini mwilini na waelewe changamoto hiyo ndiyo inayowafanya kuzaa watoto wenye changamoto.
Ngazo
amesema serikali imejenga vituo vya afya kila kona ni wajibu wa wazazi kwenda kupima afya zao
kabla ya kubeba mimba ili wajiandae na malezi ya mtoto kuanzia tumboni
nakuondokana na ulaji wa udongo wa pemba ambao unasababishwa na kukosa madini chuma mwilini.
“Utakuta mjamzito haendi kliniki mpaka mimba
ifikishe umri wa miezi saba au nane hajui maendeleo ya mtoto aliyeko tumboni
wakati mwingine anazalia nyumbani hapo unategemea utaleta kiumbe chenye utimamu
wa akili duniani kweli”amesema Ngazo
Ngazo amesema wanawake wanategemewa kuwa madaktari namba moja kwa kujua hali ya mtoto kabla ya kuzaliwa daktari hospitalini yeye wa pili kukuelekeza wakifanya hivyo wataweza kuokoa vifo vya watoto na kuondoa changamoto zingine zenye kuzuilika.


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464